Serikali yaombwa iwekeze kwenye ngoma za asili...soma habari kamili na Matukio360..#share

Na mwandishi wetu
WASANII wa ngoma za asili Mkoani Mbeya wameiomba Serikali iwawezesha na kutangaza ngoma za asili za makabila ya mikoa ya nyanda za juu kusini



 Wasanii wa ngoma ya asili ya kabila la wangoni wakitumbuiza  katika viwanja vya Ruanda Nzovwe mkoani Mbeya

Akizungumza na Matukio360 jijini Mbeya Mkurugenzi wa Kikundi cha asili cha kabila la wangoni,  Seif  Seif amesema ngoma za asili za makabili ya mikoa ya kusini hazitambuliki  vizuri katika mikoa mingine na nje ya nchi.

“Nyanda za juu kuna ngoma za asili za makabila mengi sasa Serikali kupitia kwa viongozi hususan wabunge wawekeze katika vikundi vya mila na desturi na si kuzitumia  wakati wa kampeni za uchaguzi.”

"Mfano mzuri kwa Naibu Spika Tulia Ackson aliandaa mashindano ya kushindanisha ngoma za  asili wilayani Rungwe na hiyo ni njema  kwa
wazawa na kujitengenezea upendo mkubwa kwa wanarungwe."amesema.


Seif amesema njia pekee ni kuboresha utamaduni wa mtanzania mahala popote, makabila yatambuliwe na kuheshimika  na kwamba itajenga na kuboresha zaidi uzalendo nchini.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search