Afungwa jela maisha kwa kubaka mtoto..soma habari kamili na Matukio360...#share

Na mwandishi wetu
MAHAKAMA ya Wilaya ya Ilala imemhukumu Mkazi wa Dar es Salaam Faraja Said kwenda jela maisha kwa kosa la kumbaka mtoto wa miaka 8.

Imedaiwa mtuhumiwa alifanya kosa hilo Disemba mwaka 2015. Hakimu Mkazi Mfawidhi, Ritha Tarimo akitoa hukumu hiyo amesema mahakama imejiridhisha na ushahidi uliotolewa ambapo ilikuta mshtakiwa ana kesi ya kujibu.

Katika ushahidi uliotolewa na shahidi wa kwanza ambaye ndio mtoto aliyebakwa alieleza namna mshtakiwa huyo alivyombaka na kuonesha kuwa kweli mshtakiwa alifanya kosa hilo.

Ilidaiwa mahakamani hapo kuwa Daktari wa hospitali ya Amana alithibitisha mtoto huyo alibakwa ambapo alipomchukua vipimo waligundu  ameingiliwa kumwili na kukuta michubuko.

Hakimu alimuuliza mshtakiwa kama ana chochote cha kuiambia Mahakama kabla ya kutoa adhabu ambapo alijibu anaomba apunguziwe adhabau ana Mke na  watoto wanamtegemea.

Mwendesha mashtaka Anuciantha Leopold amesema hakuna kumbukumbu za makosa ya nyuma ya mshtakiwa hivyo apawe adhabu ili iwe fundisho kwake na kwa wengine wenye tabia kama yake. Hakimu alimuhukumu kwenda jela maisha.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search