Waziri Mwakyembe ateta na viongozi wa dini...soma habari kamili na Matukio360..#share
Na Hussein Ndubikile
VIONGOZI wa Madhehebu ya
Dini nchini wametakiwa kuwakemea waamini wao waache kuvaa mavazi yasiyofaa
wakiwa madhahabuni badala yake wawafundishe matendo mema yanayompendeza Mungu
na yanayodumisha maadili na uzalendo wa nchi.
Waziri Dk Mwakyembe akiwa na viongozi wa dini
Hayo yamesemwa leo jijini
Dar es Salaam na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison
Mwakyembe katika mkutano uliomkutanisha na Viongozi wa Madhehebu ya dini kwenye
Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Mwalimu Nyerere.
Amesema maadili ya jamii
yamekuwa yakimomonyoka kutokana viongozi hao kuyafumbia macho hata pale kwenye
nyumba na kwamba wanatakiwa kuwakemea kwa kuwafundisha yale yote yanayomchukiza
na kumpendeza Mungu.
“ Viongozi wote wa dini
mnatakiwa kukemea waamini wasivae mavazi yasiyofaa kimaadili siku zote matatizo
makubwa yanaanza polepole tukichelelwa kuwakumbusha waamini na vijana wetu
wanapotea,” amesema.
Amebainisha kuwa viongozi
wanatakiwa kuwakumbusha waamini wajibu wa kulipa kodi, kufanya kazi kwa bidii,
kutunza mazingira, uaminifu, uadilifu, uwajibikaji na kutii mamlaka na kulinda
rasilimali za nchi.
Amesisitiza kuwa Serikali
itaendelea kuchukua hatua kwa yeyote atakayebainika kutoa lugha za kichochezi
lengo likiwa kuiokoa nchi isiingie kwenye janga la machafuko kama yanavyotokea
katika mataifa mengine ya Afrika.
Amewapongeza wasanii wa
nyimbo za Injili na Kaswida kwa kutumia lugha sanifu na kuvaa mavazi ya staha
wakiwa kazini.
Kwa upande wake Sheikh Mkuu
wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum amewahimiza viongozi wenzake
kutoyanyamazia maovu huku akiongeza mwenyezi
Mungu humpenda mtu anayetenda mema.
Naye Mchungaji Antonio
Fernandes ambaye pia ni Mmiliki wa Kituo cha Runinga cha ATN amesema kila
mwananchi ana wajibu kufanya kila ili kujiletea maendeleo na kuikomboa nchi
kiuchumi.
Ameiasa jamii kuacha
kuitumia vibaya mitandao ya kijamii vibaya badala yake waitumie kutafuta fursa
mbalimbali zinazopatikana kwenye mitandao hiyo.
Mlezi wa Jumuiya na taasisi
za madhehebu ya dini, Mary Rhoida amewakumbusha viongozi kuwa na utaratibu wa
kutatua migogoro katika ngazi za chini
ili kuepuka migongano inayoweza kujitokeza.
Mwakilishi kutoka Rita, Lina
Msangi amesema viongozi wa dini wana wajibu wa kuwasisitiza na kuwakumbusha
waamini wao kuwa na utamaduni wa kushughulikia vyeti vya kuzaliwa na kufuatilia
masuala ya mirathi.
No comments:
Post a Comment