Zitto, Nassari wamjibu msemaji mkuu wa Serikali...soma habari kamili na Matukio360..#share

Na Mwandishi wetu
SIKU chahe baada ya Serikali kulichkulia hatua za kisheria gazeti la Tanzania Daima ikidai inaendeleza kuandika habari za uongo, mbunge Zitto Kabwe na Joshua Nassari wamejibu mapigo kwa nyakati tofauti kuhusu sakata hilo.

Mbunge wa Kigoma mjini, Zitto Kabwe
Jana msemaji mkuu wa serikali na mkurugenzi mkuu wa Idara ya Habari Maelezo, Dk Hassan Abass alitangaza kulifungia kwa siku 90 gazeti la Tanzania Daima.

Leo kwa nyakati tofauti mbunge wa Kigoma mjini Zitto Kabwe amemjibu Dk Abass kuwa naye asubiri kupewa tuzo kutokana na kufungia ovyo magazeti.

‘Unafurahia sana kufunga magazeti. Na wewe upewe nishani ya kufungia magazeti mengi zaidi katika muda mfupi tangu Uhuru 1961.’ Ameandika Zitto ambaye pia ni kiongozi mkuu wa chama cha ACT-Wazalendo katika ukurasa wake wa Tweeter

Naye mbunge wa Arumeru Mashariki Joshua Nassari katika ukarasa wake wa Tweeter ameandika ‘ Ni sahihi barua za @Msigwa Gerson kuwa ni typing errors ila wengine ni kosa la kuchukuliwa hatua.’


Kwa kipindi cha miaka miwili tayari serikali imeshafungia magazeti manne ambayo ni Mseto, Mwanahalisi, Raia Mwema na Tanzania Daima

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search