Afya ya Harbinder Sethi bado 'tete'...soma habari kamili na Matukio360...#share
Na mwandishi wetu
MAHAKAMA ya Hakimu
Mkazi Kisutu imeelezwa kuwa mshtakiwa Harbinder Sethi pamoja na kupelekwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili(MNH) na
kuchukuliwa vipimo bado hajapata majibu wala matibabu yoyote na afya yake inazidi
kuzoofika.
Harbinder Sethi wa pili kutoka kushoto
Wakili wake, Alex
Balomi leo ameeleza hayo mbele ya Hakimu
Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi Mara baada ya
Wakili wa Serikali Mwandamizi, Kishenyi
Mutalemwa kudai upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika na akaomba ipangiwe tarehe
nyingine.
Kishenyi
baada ya kueleza hayo, Wakili Balomi
alieleza kuwa kwa kiasi fulani upande wa Mashtaka umetekeleza amri ya
mahakama kwa kumpeleka Muhimbili na kuchukuliwa vipimo lakini hajapewa majibu
na wala hajatibiwa hadi sasa.
Amedai
kuwa lile puto alilowekewa tumboni Sethi linatakiwa kubadilishwa mwishoni kwa
mwezi huu, lisipobadilishwa litageuka kuwa sumu na kuhatarisha uhai wake.
Aliendelea
kudai kuwa daktari aliyechukua vipimo ampatie majibu ili aweze kujua hali ya
afya yake ikoje.
Wakili
Kishenyi baada ya kutolewa kwa maelezo hayo alidai kuwa wao wamekwisha
tekeleza amri ya mahakama, hawana cha
kufanya zaidi kwa sababu majibu ni siri ya magonjwa na Daktari.
Mwendesha
Mashtaka Mwandamizi wa Takukuru, Leonard Swai yeye naye alidai kuwa suala la
majibu ni suala la magonjwa na Daktari.
Baada
ya kutolewa kwa maelezo hayo, Hakimu Shaidi Alisema amri ya mahakama
imetekelezwa ambapo mshtakiwa alipelekwa Muhimbili, na siyo jukumu la mahakama
kuingilia kazi ya Daktari hivyo alishauri mawakili wa upande wa utetezi wafuate
utaratibu.
Kesi
imeahirishwa hadi Novemba 10,2017 kwa ajili ya kutajwa na kuusisitiza upelelezi
ukamilishwe.
Wakili
wa mshtakiwa James Rugemalira, Respicius
Didas aliunga mkono hoja za wakili Balomi na kuongeza kuwa kuna suala la ucheleweshwaji wa
upelelezi katika kesi hiyo.
Washtakiwa
hao walifikishwa mahakamani hapo kwa Mara ya kwanza Juni 19,mwaka 2017 na wapo ndani hadi sasa.
Katika
kesi hiyo, washtakiwa Harbinder Singh
Sethi na James Burchard Rugemarila
wanakabiliwa na mashtaka 12 ya uhujumu uchumi kwa Kula njama, kujihusisha mtandao wa uhalifu ,
kighushi, kutoa nyaraka za kughushi na
kujipatia fedha kwa njia za udanganyifu.
Pia
wanakabiliwa na mashtaka matano ya
kutakatisha fedha pamoja na
kusababisha hasara ya USD 22, 198,544.60 na Sh 309,461,300,158.27.
Rugemarila
ni Mkurugenzi wa VIP na mmiliki mwenza
wa zamani wa IPTL na Sethi ni Mwenyekiti Mtendaji wa PAP ambapo wanadaiwa kutenda makosa hayo kati ya oktoba
18 ,2011 na Machi 19 , 2014.
No comments:
Post a Comment