Mbunge Ester Bulaya Chadema, Adai Watu Wasiojulikana Kuhatarisha Maisha yake..Soma Habari Kamili na Sikiliza Sauti Akithibitisha Hilo na Matukio360..#share


MBUNGE wa Jimbo la Bunda Mjini kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Ester Bulaya, amesema maisha yake yapo hatarini kutokana na kufuatiliwa na watu ambao anahisi sio wazuri huku wakiwa wamevalia mavazi ya ninja, nyumbani kwake wilayani Bunda.
Kauli hiyo amietoa wakati akizungumza  na mwandishi wa kituo kimoja cha televisheni hapa nchini, amesema kwamba watu hao walimfuata nyumbani kwake wakiwa na gari ya Noah huku wamevalia kinija, bahati nzuri hakuwepo nyumbani hivyo ndugu zake wakamwambia asirudi nyumbani siku hiyo.

Aidha Bulaya amefafanua kwamba watu hao walizunguka kwa baadhi ya ndugu zake akiwemo bibi yake na kumkosa, lakini alienda kutoa taarifa polisi na mkuu wa kituo kuanza kufuatilia suala hilo, lakini haikuchukua muda akahamishwa kituo cha kazi.



Msikilize Hapa Akibainisha Taarifa Hiyo

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search