Dk Mwaiselage:Tezi dume haipimwi kwa kidole..soma habari kamili na Matukio360..#share

Salha Mohamed
MKURUGENZI Mtendaji wa Taasisi ya Saratani ya Ocean Road, Dk.Julius Mwaiselage amesema saratani ya tezi dume haipimwi kwa kutumia kidole kama ambavyo taarifa mbalimbali zinavyoeleza.


Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Ocean Road, Dk.  Julius Mwaiselage akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam juu ya matembezi ya hisani ya kuhamasisha Uchunguzi wa saratani ya matiti yatakayofanyika kesho yatakayoanzia katika viwanja vya Taasisi hizo.
Amesema hayo leo jijini Dar es Salaam, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu matembezi ya hisani ya kuhamasisha uchunguzi wa mapema wa saratani  ya matiti.

Amesema wananchi wamekuwa na dhana potofu ya namna ya kupima saratani ya tezi dume na kuwafanya wanaume kushindwa kujitokea katika upimaji ili kuanza matibabu.

“Watu hupotosha namna ya upimaji tezi dume, Tanzania imeweka mwongozo wa kupima tezi dume ambapo wanapima kupitia damu,”amesem.
Amesema mwanaume hufika kituo cha kutolea huduma za afya na kupima damu kama ambavyo mgonjwa wa malaria au HIV anavyopimwa.

Amesema endapo mgonjwa atajulikana na ugonjwa huo daktari atachukua hatua nyingine ya matibabu zaidi lakini si kwa namna ambavyo wananchi wanavyosema matibabu yake kwenye mitandao ya kijamii.

Dk. Mwaiselage amewataka wananchi kuwa na utaratibu wa kupima saratani mara kwa mara kwani huduma hiyo hutoewa bure kwenye vituo 460 hapa nchini.

Amesema taasisi hiyo ilihudumia wagonjwa 27,907 ambapo wagonjwa wapya wa saratani 6,338 na wale wa marudio waikuwa 21,569.

“Taasisi ilifanya uchunguzi wa saratani ya matiti na shingo ya kizazi kwa watu 9,028 ambapo kati yao 1,123 walikutwa na dalili za awali za saatani ya matitina shingo ya kizazi,”amesema.

Ameongeza kuwa taasisi hiyo ilifanya uchunguzi wa satarani ya tezi dume kwa wananume 534 ambapo kati yao 27 walikutwa na dalili za awali za saratani.

Amesema kwenye taasisi hiyo wagonjwa wa saratani  wamekuwa wakiongezeka kila mwaka hadi kufikia mil 14.1 huku mil 8.8 hufariki kila mwaka kwa mujibu wa Shirika la Afya duniani ya mwaka 2015 ikisababishwa na sababu mbalimbali.

Mkurugenzi wa Kinga Hospitali ya Agakhani, Dk. Crispin Kahesa amesema saratani haichagui jinsia ambapo hata waname huwapata ambapo serikali imejenga uwezo wa rasilimali watu katika kuongeza tiba.


Taasisi hiyo inatarajia kufanya matembezi ya hisani ya kuhamasisha saratani ya matiti kesho yatakayoanzia katika taasisi hiyo huku mgeni rasmi akiwa Waziri wa Afya , Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search