Kesi ya Jamali Malinzi 'kizungumkuti'..soma habari kamili na Matukio360..share

 Na mwandishi wetu
 WAKILI, Richard Rweyongeza anayemtetea  rais wa zamani wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania(TFF), Jamal Malinzi na wenzake umeiomba  Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kumuita  Mkurugenzi wa Mashtaka ya Jinai (DPP)  kueleza ni kwanini jalada la kesi hiyo lipo ofisini kwake kwa muda wa siku 37.


Rais wa zamani wa TFF, Jamali Malinzi wa pili kutokata kulia akiwa Mahakamani
Amewasilisha ombi hilo leo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri kufuatia Mwendesha Mashtaka Mwandamizi wa Takukuru, Leonard  Swai kudai  upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika na kuomba ipangiwe tarehe nyingine.

Baada ya kutolewa kwa maelezo hayo, Wakili Rweyongeza alieleza kuwa upande wa Mashtaka awali waliomba wiki mbili ili walete taarifa kamili kuhusu jalada lililopo kwa DPP.

Katika maelezo ya Swai hatujasikia taarifa ya DPP kuhusu jalada hilo na kwamba wao walifuatilia.Aliongeza kudai kuwa wanasita kusema ni matumizi mabaya ya sheria ama ni matumizi mabaya ya mamlaka ya DPP lakini hakuna lugha nzuri zaidi inabidi waseme hivyo.
  
Wakili Rweyongeza aliomba mahakama imuite DPP mahakamani hapo ili afike kueleza kuna kitu gani ili haki ionekane inatendeka kwa muda anajukumu la kisheria la kuzingatia haki na kutenda kazi yake kwa kuzingatia haki

Wakili wa utetezi, Abrahamu Senguji alidai kuwa na yeye alilifuatilia jalada hilo katika ofisi ya DPP lakini hakupata majibu yaliyomuonesha kuwa DPP yupo makini hasa  katika kesi hiyo.

Hivyo alidai kuwa kutokana na kutokutenda kazi na kutokutenda Haki DPP mwenyewe aitwe mahakama ni hapo kueleza ni kwanini jalada hilo limekaa ofisini kwake kwa muda wa mwezi mmoja na siku saba.

Pia aliomba mahakama nitumie mamlaka yake kuzuia manyanyaso kwa washtakiwa na iingilie kati katika suala hilo ili Haki ionekane inatendeka.

Vinginevyo upande wa Mashtaka wawabadilishie Mashtaka washtakiwa wapate dhamana ili wao waendelee na upelelezi.
Baada ys kueleza hayo, Swai alidai kuwa ofisi ya DPP inapokea majalada kutoka nchi nzima kwa ajili ya kuyatolea maelekezokuhusuana na uchunguzi.

Alidai kuwa makosa ya kughushi yanahitaji utaalam katika kuyathibitisha na yanachukua muda mrefu katika uchunguzi.

Aliongeza katika hili lilipelekwa kwa ajili ya kupitiwa ili atoe kibali liendelee ama upelelezi zaidi ufanyike ama hakuna ushshidi wa kutosha ifutwe.

Swai aliongeza kuwa jalada la kesi hii limerejeshwa kwa ajili ya uchunguzi zaidi lakini awajapewa taarifa ya maandishi ya kiofisi ndiyo maana hawakulisema hilo na akaomba ahirisho.
Rweyongeza alidai kuwa jalada la kesi hiyo tangu Oktoba 5,2017 jalada lipo kwa DPP.

Hakimu Mashauri atatoa uamuzi wa hoja hizo Novemba 10,2017. Katika kesi hiyo, washtakiwa wengine wanaokabiliwa na kesi hiyo ni Katibu Mkuu wa TFF, Mwesigwa Selestine na Mhasibu wa shirikisho hilo, Nsiande Mwanga.

Washtakiwa hao wanakabiliwa na mashtaka 28, yakiwamo ya utakatishaji fedha wa Dola za Marekani, 375,418.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search