Waziri Ummy kuchangia damu wagonjwa wa saratani..soma habari kamili na matukio360..#share

Na Salha Mohamed
WAZIRI wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu ataongoza matembezi ya hisani  kuhamasisha na kutoa elimu ya saratani ya matiti na kuchangia damu.


Waziri Ummy Mwalimu
Matembezi hayo yatafanyika Oktoba 28, 2017 kuanzia Taasisi ya Ocean Road hadi Stesheni na wananchi wametakiwa kujitokeza  kwa wingi kuchangia damu kwa wagonjwa wenye saratani.

Akizungumza na Matukio360, Meneja Uchunguzi wa satarani na Elimu kwa Umma taasisi ya Ocean Road, Dk Maguha Stephano amesema asilimia 12 ya wagonjwa wapya wanaofikishwa katika taasisi hiyo wanaumwa saratani ya matiti.

"Mwaka 2006 hadi 2015 inakadiriwa wagonjwa 6000 walipimw kati yao wagonjwa 900 wanasaratani ya matiti, "amesema.

Amesema  taasisi hiyo kwa sasa imepokea wasichana wenye miaka 25 wakiwa na saratani ya matiti hali inayochangiwa na vihatarishi kadhaa.

Amesema sababu za kimaumbile ni moja ya vihatarishi vya saratani,  wanawake ndiyo waathirika zaidi na kwamba wanaume ni hatari zaidi.

Dk Stephano amesema wananchi wajitokeze kwa wingi  katika matembezi hayo na kuchangia damu wagonjwa wa saratani kwa kuwa matibabu yao huitaji damu nyingi.

"Kutakuwa na uchunguzi wa saratani ya matiti, utoaji damu kwa wagonjwa wa saratani kwani huwa na upungufu wa damu hasa wale wenye vidonda vinavuja damu, "amesema.

Amesema wapo wagonjwa wenye saratani ya damu hivyo huwa na uhitaji wa damu mara kwa mara.



About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search