Makonda atahadharisha wakazi Dar es salaam... soma habari kamili na matukio360..#share
Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda ametoa tahadhari kwamba mvua kubwa zaidi zitanyesha Dar kuanzia tarehe 1 November.
“Hali hii ya mvua itaendelea kuwa kubwa zaidi na tumeambiwa na Wataalamu kwamba inakuja nyingine kubwa zaidi kuanzia tarehe moja hivyo tujihadhari”
Pamoja na tahadhari hiyo, Makonda ameligiza Jeshi la Wananchi wa Tanzania JWTZ kujenga daraja la muda (daraja la Malecela) ambalo liliharibiwa na mvua zilizonyesha.
“Nimewaagiza JWTZ watakuja kujenga daraja la muda ili magari yapite wakati TANROADS wakijipanga kwa ajili ya ujenzi wa muda mrefu kurudisha miundombinu kama inavyotakiwa”
‘Nafahamu kuna nyumba zaidi ya 200 ziko katika sehemu hatarishi Kinondoni, zile 190 zilizobomoka pia tuendelee kushirikiana na Wadau kuhakikisha tunapata hifadhi huku tukijipanga kuwa na sehemu salama zaidi”
“Kamati ya maafa ya Mkoa imefanya kazi nzuri toka jana kwa kuokoa Wananchi wengi kwenye maeneo tofauti na kwakweli bila wao tungekua na idadi kubwa ya watu waliokufa”
“Hali hii ya mvua itaendelea kuwa kubwa zaidi na tumeambiwa na Wataalamu kwamba inakuja nyingine kubwa zaidi kuanzia tarehe moja hivyo tujihadhari”
Pamoja na tahadhari hiyo, Makonda ameligiza Jeshi la Wananchi wa Tanzania JWTZ kujenga daraja la muda (daraja la Malecela) ambalo liliharibiwa na mvua zilizonyesha.
“Nimewaagiza JWTZ watakuja kujenga daraja la muda ili magari yapite wakati TANROADS wakijipanga kwa ajili ya ujenzi wa muda mrefu kurudisha miundombinu kama inavyotakiwa”
‘Nafahamu kuna nyumba zaidi ya 200 ziko katika sehemu hatarishi Kinondoni, zile 190 zilizobomoka pia tuendelee kushirikiana na Wadau kuhakikisha tunapata hifadhi huku tukijipanga kuwa na sehemu salama zaidi”
“Kamati ya maafa ya Mkoa imefanya kazi nzuri toka jana kwa kuokoa Wananchi wengi kwenye maeneo tofauti na kwakweli bila wao tungekua na idadi kubwa ya watu waliokufa”
No comments:
Post a Comment