BoT, NBS wamjibu Zitto...Soma habari kamili na Matukio360..#share


Na Abraham Ntambara

BENKI Kuu ya Tanzania (BoT) imekanusha taarifa zilizotolewa na Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo na Mbunge wa Kiogoma Mjini Zitto Kabwe kuhusu takwimu za pato la taifa, ujazi wa fedha na mfumuko wa bei ambazo anadai zinatia mashaka.

Mkurugenzi wa Sera na Tafiti toka Benki Kuu, Johnson Nyella (kushoto)akifafanua jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati akikanusha taarifa za upotoshaji kuhusu takwimu za pato la taifa mapema hii leo jijini Dar es Salaam, kulia ni Meneja wa Takwimu za Pato la Taifa toka Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Daniel Masolwa.

Wakizungumza  kwa pamoja na  waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo Benki Kuu ya Tanzania (BoT) na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) , wamesema taarifa hizo ni za uongo, upotoshaji na kuwataka wananchi wazipuuze.

Hivi karibuni Zitto alidai kuwa na mashaka juu ya takwimu za ukuaji wa pato la taifa na mfumko wa bei kwenye robo iliyoishia Juni, 2017 kuwa ulipaswa kuwa asilimia 0.1 na siyo asilimia 5.7 kama ilivyochapishwa katika ripoti ya robo ya mwaka ya Benki Kuu.

Mkurugenzi wa Sera na Tafiti kutoka BoT Johnson  Nyella, amesema  ukuaji wa asilimia 5.7 alioutaja kiongozi huyo wa ACT-Wazalendo ulikuwa wa robo ya kwanza ya mwaka 2017 na siyo robo ya pili.

“Ripoti ya Benki Kuu aliyoitumia ilikuwa na takwimu za hadi robo ya kwanza mwaka 2017, kwani ilichapishwa kabla ya takwimu za pato la taifa za robo ya pili hazijatolewa na Ofisi ya Takwimu ya Taifa (NBS) . Ukuaji wa pato halisi la taifa katika robo ya pili ya mwaka 2017 ulikuwa asilimia 7.8,” amesema Nyella.
Aidha amedai kuwa Zitto amekokotoa ukuaji wa pato la taifa anaodai kuwa sahihi kwa kuangalia tofauti kati ya ongezeko la ujazi wa fedha (m) na mfumuko wa bei (p).
Kwa upende wake Meneja wa Takwimu za Pato la Taifa (NBS) Daniel Msolwa, akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa NBS, amesema Zitto anatakiwa kufahamu kuwa takwimu za robo ya mwaka hurekebishwa (revised) baada ya kupatikana kwa taarifa za kina za uzalishaji wa bidhaa na huduma katika nchi ikiwa ni pamoja na vitabu vya mahesabu vilivyokaguliwa.
Meneja wa Takwimu za Pato la Taifa kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Daniel Masolwa (kulia) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati akikanusha taarifa za upotoshaji kuhusu takwimu za pato la taifa mapema hii leo jijini Dar es Salaam, kushoto ni Mkurugenzi wa Sera na Tafiti toka Benki Kuu, Johnson Nyella
“Ni vema Zitto Kabwe akawa makini na uchambuzi anaofanya na siyo kuupotosha umma kwa kutumia kichaka cha takwimu au mjadala wa kufurahisha umma. Kama hana ufahamu ni bora angeuliza aelimishwe kabla ya kuendelea na uchambuzi wake na hatimaye angeweza kuja na ripoti yenye mashiko,” amesema Msolwa.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search