Mauaji Kanumba ushahidi waanza kutolewa dhidi ya Lulu...soma habari kamili na Matukio360...#share

Na Mwandishi wetu
SETH Bosco(30) amedai muigizaji Elizabeth Michael 'Lulu' aliondoka na kumuacha Steven Kanumba peke yake baada ya kuanguka

Elizabeth Michael maarufu Lulu
Bosco ambaye ni mdogo wa marehemu Kanumba amesema hayo leo jijini Dar es Salaam  katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, mbele ya Jaji Sam Rumanyika wakati akitoa ushahidi wake
Shahidi huyo wa kwanza wa upande wa mashtaka kwa kesi  hiyo ya mauaji ya bila kukusudia  amedai licha ya kumweleza Lulu abaki na Kanumba, yeye alipomfuata daktari aliondoka na kumuacha peke yake.
Awali Lulu alikumbushiwa mashtaka yake ya kwamba  April, 2012 huko Sinza Vatican wilayani Kinondoni alimuua bila kukusidia Kanumba, Lulu alikana shtaka hilo.
Akiongozwa na Wakili wa serikali Faraja  George, Bosco amedai baada ya kupata taarifa za kudondoka kwa Kanumba kutoka kwa Lulu alimpigia simu daktari wao aliyemtaja kwa jina la Paplas ambaye alimtaka kwenda kumchukua Hospitalini kwake na kwa kuwa hakukuwa na usafiri aliwasha gari na kumfuata na kumuomba Lulu abaki na Kanumba.
"Wakati narudi na Dokta, Lulu alinipigia simu akasema nimemuwekea maji kifuani Kanumba  lakini haamki nikamwambia nisubiri lakini nilipofika sikumkuta" amesema
Alidai baada ya Dokta kufika na kumpima alishauri apelekwe Muhimbili, kwa msaada wa jirani  aliyemtaja kwa jina la Baraka walimbeba Kanumba na kumuingiza kwenye gari hadi Muhimbili.
Alidai wakati wanaangaika kumuingiza Kanumba kwenye gari, mama mwenye nyumba alisikia akafungua mlango aliposikia tatizo nae aliwasha gari lake na kuwasindikiza, ambapo walienda moja kwa moja Emergency na baada kumfanyia Kanumba uchunguzi Dokta aliwaambia amefariki na watafute taratibu za polisi
Amedai  walienda Kituo cha Polisi Urafiki, wakiwa huko Lulu alikuwa akimpigia Dk Paplas simu ndipo polisi wakamuomba Dokta aweze kuwasaidia kumpata Lulu  ambapo asubuhi ya Aprili 7, baada ya wao kumaliza kuhojiwa Lulu alakamatwa.
Akielezea jinsi tukio  hilo alidai, Aprili 4 mwaka 2012 alishinda nyumbani na kaka yake toka asubuhi na ilipofika mida ya saa kumi jioni, Kanumba alimuomba asitoke na wangetoka pamoja usiku wa saa sita.
Alidai ilipofika Saa sita kasoro za usiku Kanumba alimwambia wajiandae watoke, ambapo yeye alikuwa wa Kwanza kumaliza kujiandaa lakini alipotoka chumbani kwake akielekea sebuleni, alikutana na Kanumba akipita kwenye koridoni huku akiwa amevalia taulo kuelekea sebuleni, akipaka Mafuta kichwani na kwamba sebuleni kwa nje kulikuwa na Gari la Lulu.
Alidai kuwa, Kanumba ndiye alimfungulia mlango lulu, waliingia wote ndani akiwa chumbani kwake ambako alirudi kumsubiria Kanumba huku mlango wake ukiwa wazi kidogo, wakati wakitembea Koridoni kuelekea chumbani kwa  Kanumba alisikia wakigombana huku Kanumba akimuuliza lulu kwa nini anaongea na boyfriend wake mbele yake.
Aliendelea kudai kuwa muda wote huo walikuwa wakivutana, Lulu akitaka kutoka nje na Kanumba akimvutia ndani mara waliingia chumbani na mlango ukafungwa.
" Nilisikia sauti za kupigana na muda mfupi kidogo Lulu alifungua mlango na kuja chumbani kwangu akasema, Kanumba amedondoka sijui amekuwaje"alidai
Alidai aliondoka hadi chumbani kwake, alimkuta Kanumba amedondoka kwa kuegemea ukuta huku akiwa hawezi kupumua, (amesafocate), alimchukua na kumlaza chini kisha akampigia simu Dr Paplas  na Mazingira ya chumba hicho cha kaka yake yalikuwa ya kawaida kama siku zote.
Alidai baada ya hapo aliwasha gari  na kwenda kumchukua Dr ndipo Lulu akanipogia simu na kusema Kanumba haamki.
Wakili wa utetezi, Peter Kibatala alimuuliza Shahidi kama ushahidi aliotoa mahakamani unafanana na maelezo  waliyoyatoa polis ambapo alijibu ndio.
Kibatala alimuuliza shahidi huyo ni wapi aliwaeleza polisi kuwa alimuacha mshtakiwa Lulu peke yake na Marehemu Kanumba wakati anaenda kumtafuta Dr, Paplas alisem hakuwaeleza.
Alidai kuwa yeye alikuwepo kwenye postmotam ya kawaida na wala hakuwepo wakati wakichukua sampuli za mwili kupeleka maabara.
Jaji Manyika aliarisha kesi hiyo hadi leo ambapo itaendelea na ushahidi wa Dr Paplas ambaye jana alishindwa kutoa ushahidi kwasababu alikuwa hajiskii vizuri
February 18/2014  akisomewa maelezo ya awali, Lulu alikiri mahakamani kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Kanumba na pia kuwa kulikuwepo na ugomvi baina yao siku ya tukio la kifo cha mwigizaji huyo.
Kwa mara ya kwanza Lulu alipandishwa kizimbani Aprili 11,2012 mbele ya   Hakimu mfawidhi wa wakati huo wa Mahakama ya  Hakimu Mkazi Kisutu, Augustina Mbando ambapo alisomewa mashitaka ya mauaji.
Lulu aliachiwa kwa dhamana Januari 29, 2013 baada ya kesi hiyo kubadilishwa hati ya mashitaka kutoka kwenye kesi ya mauaji kwenda mauaji ya bila kukusudia ambapo badiliko hilo lilimpa nafasi ya kupata dhamana.

Katika kesi ya msingi namba 125 ya mwaka 2012, inadaiwa kuwa Aprili 7,  2012 Sinza Vatican jijini Dar es Salaam, Lulu alimuua Kanumba bila kukusudia.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search