Zitto azidi kukimbiwa, Mwingamba wenzake 10 wajiunga CCM..soma habari kamili na Matukio360..#share

Na Abraham Ntambara
ALIYEKUWA Mwenyekiti wa Kamati ya Kampeni na Uchaguzi Taifa ya Chama Cha ACT Wazalendo Samson Mwigamba na wenzake 10 wamejiunga na CCM.

Samson Mwigamba na baadhi wa wanaACT-Wazalendo Leo jijini Dar es Salaam wakitangaza kujiunga na CCM

Hatua hiyo inakuja ikiwa ni siku chache Mwigamba kung'atuka nafasi yake hiyo katika chama hicho na kudai angebaki kuwa mwananchama wa kawaida akidai kuna mambo ndani ya chama hicho hayaendi sawa.

Mwigamba alidai alijitahidi  kuongea na viongozi wakuu wa chama hicho kuhusu mambo mbalimbali lakini  hayatendeki wala kufanyiwa kazi hivyo kufanya maamuzi hayo ili kutopingana nao na aweze kupata nafasi ya kuhoji baadhi ya mambo ndani ya chama

Lakini leo jijini Dar es Salaam katika mkutano wake na waandishi habari ametanga kujiunga na CCM na kwamba wana ACT-Wazalendo zaidi ya kumi nao wameng’atuka kutoka chama hicho.

Viongozi hao waliotangaza kukihama chama hicho  ni Wilfred Kitumba mwenyekiti wa Act-Wazalendo mkoan Singida, Liploth Robert  Katibu wa Chama hicho mkoani Singida, Emmanuel Wilfred ofisa utawala  chama cha Act-wazalendo Makao makuu.

Wengine ni  Mwamtumu Mgonjwa ambaye ni ofisa wa Sheria wa chama hicho Taifa, Peter Mwambeja  mtunza hazina wa Chama, Dasan Ullotu ambaye ni Katibu wa Chama Mkoani Arusha, Wilson Laizer Katibu wa Chama hicho Wilaya ya Arusha.

Wengine ni Nakamia Wazael ambaye ni Mwenyekiti wa chama hicho jimbo la Singida Mjini, na Denson Chembo Katibu wa chama uadalifu Taifa.

Miongoni mwa sababu za kujiondoa kwao ni kuwa chama kimekosa dira na uelekeo na kimekuwa ni cha uanaharakati.

“Kwa sasa tumeamua kung’atuka ACT-Wazalendo na tunajiunga CCM kwa kuwa kinaanza kutekeleza misingi ya Azimio la Arusha ambalo sisi ndio ilikuwa dira yetu,” amesema Mwantumu.




About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search