Mauzo ya hisa DSE yashuka...soma habari kamili na Matukio360..#share
Salha Mohamed
THAMANI ya mauzo ya hisa katika soko la hisa Dar es Salaam (DSE),imepungua kutoka bilioni 30 Oktoba 13 hadi bilioni 23, Oktoba 20, 2017.
THAMANI ya mauzo ya hisa katika soko la hisa Dar es Salaam (DSE),imepungua kutoka bilioni 30 Oktoba 13 hadi bilioni 23, Oktoba 20, 2017.
Afisa mwandamizi wa masoko DSE, Mary Kinabo Hata hivyo Ofisa Mwandamizi wa masoko DSE, Mary Kinabo amesema "Idadi ya hisa zilizouzwa na kununuliwa imepanda kutoka hisa milioni 2.5 ya Oktoba 13, 2017 hadi hisa mil 2.8 kwa Oktoba 23, 2017."
Kampuni zilizoongoza katika mauzo ya hisa ni kampuni ya Bia (TBL) kwa asilimia 89, Kiwanda cha Sigara(TCC) asilimia kumi, na Benki ya CRDB asilimia moja.
Kinabo ameongeza kuwa ukubwa wa mtaji wa kampuni
zilizoorodheshwa katika soko umepanda kwa bilioni 463 kutoka trilioni 20.4 kwa wiki iliyopita hadi trilioni 20.9 hadi Oktoba 23,
2017.
"Ukubwa wa mtaji wa kampuni za ndani umeongezeka kwa bilioni 205 kutoka trilioni 9.96 hadi kafika trilioni 10.2 wiki
hii...hii ni kutokana na kupanda kwa bei ya hisa za TCC kwa asilimia saba, TBL asilimia tatu na DSE kwa asilimia mbili.
Ameongeza kuwa kiashiria cha kampuni zote zilizoorodheshwa
katika soko (DSEI) kimepanda kwa pointi 48 kutoka pointi 2,124 hadi 2,172
kufikia pointi kutokana na kupanda kwa bei za hisa za Uchumi Supermarket
Ltd (USL) kampuni Kenya Airways (KA) na Acacia (ACA).
Amesema kiashiria cha sekta ya viwanda (IA) kimepanda kwa
pointi 193 kutoka pointi 5,187 hadi pointi 5,380 huku kiashiria cha huduma
za kibenki na kifedha (BI) kimeshuka kwa pointi 16 kutoka pointi 2514
hadi pointi 2498.
Kinabo amesema mauzo ya hati fungani Oktoba 20, 2017 yalikuwa
Sh. bilioni 13 kutoka Sh. bilioni 9 hadi Octoba 13 mwaka huu yametokana na
hatifungani 21 za serikali na mashirika binafsi zenye jumla ya thamani ya
Sh. bilioni 23 kwa jumla ya gharama ya Sh. bilioni 13.
No comments:
Post a Comment