Mawaziri, Wabunge kugombea tuzo...soma habari kamili na Matukio360...#share

Na Salha Mohamed

KAMATI ya utawala ya shinadano la tuzo za utekelezaji maendeleo kwa kasi ya juu kwa Wabunge na Mawaziri (THSDA) imezindua shindano la kutoa tuzo kwa wabunge na mawaziri watakaofanya vizuri katika kutekeleza majukumu yao na kuwaletea wananchi maendeleo.
Mkurugenzi mkuu wa  THSDA,   Herman Mnenuka wa pili kutoka kushota akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo

Lengo la tuzo hizo ni kupima utekelezaji wa shughuli za huduma na maendeleo kwa wananchi.

Akizungumza leo na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Katibu wa Kamati hiyo Wilson Maage amesema tuzo hizo zitapima kasi za shughuli za vingozi wa ngazi mbalimbali katika sekta na taasisi za kiserikali na taasisi hapa nchini.

“Tuzo hizo zimetokana na kuwepo wazo bunifu (intellectual property) ambalo azma yake ni kuhamasisha utekelezaji wa shughuli za huduma na maendeleo kwa wananchi wa Tanzania na kupima kasi ya utekelezaji wa shughuli hizo kwa viongozi wa ngazi mbalimbali katika sekta na taasisi za kiserikali hapa nchini,” amesema.

Amesema kufanyika kwa tuzo hizo ni kuwaweka wananchi  karibu na viongozi, kuchochea utekelezaji huduma na maendeleo kwa kasi ya juu, utawla bora na uwajibikaji wa viongozi kwa Wananchi, uhusiano mzuri kati ya serikali na Wananchi na kuimarisha furaha, utulivu na amani.

Amefafanua kuwa wahusika katika shindan hilo ni wabunge pamoja na Mawaziri ambaye ni mtetezi wa wananchi wake bila uoga akiwa ndani au nje ya Bunge.

“Sifa zingine ni awe mtendaji bora wa maendeleo yenye kuonekana, sifa ya kutoa hoja zenye tija kwa kutumia lugha ya staha bila matusi, sifa ya utekelezaji wa haraka apatapo matatizo ya Wananchi wake pamoja na sifa ya kutetea demokrasia, uhuru na kutetea wanyonge.

Mkurugenzi Mkuu wa Kamati hiyo, Herman Mnenuka amesema kuwa wananchi ndiyo nguzo kuu ya kupata kiongozi atakayepata tuzo hiyo kwani wao ndio watakaopendekeza majina ya wabunge pamoja na wamaziri wanaofaa kuwania tuzo hiyo.

Tuzo hizo ni za kwanza kutolewa hapa nchini na zitafika tamati Desemba 23 mwaka huu ambapo wananchi wanapaswa kupendekeza wabunge 15 kwa kila kigezo shindanishi, pia Wananchi watawateua Mawaziri 5 kwa kila kipengele shindanishi kwaajili ya kuingia kwenye ushindani wa tuzo hiyo na wabunge watano na Mawaziri watatu watakaopata kura nyingi kwa njia ya ujumbe mfupi (SMS) kutoka kwa wananchi wataingia katika fainali ya king’anyiro kuwania tuzo hiyo.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search