Mbunge Msigwa amuamshia dude Spika Ndugai...Soma habari kamili na Matukio360...#share

MBUNGE wa Iringa Mjini kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Mchungaji Peter Msigwa amesema anakusudia kupeleka hoja binafsi katika bunge lijalo  ya kumuondoa Spika wa Bunge Jobu Ndugai.
Mbunge wa Iringa Mjini Peter Msigwa (kushoto) na Spika wa Bunge Job Ndugai (Kulia).

Amesema hayo leo kupitia moja ya mtanadao wake wa kijamii na kubainisha kuwa atapeleka hoja hiyo kwenye bunge linalotarajia kuanza Novemba 7 mwaka huu.

Msigwa amefafanua kwa kusema kuwa atafanya hivyo kwa kuzingatia kanuni ya 137 ya kanuni za kudumu za Bunge.

"Ninakusudia kupeleka hoja ya kumuondoa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano Tanzania Mhe. Job Ndungai, kwa kuzingatia Kanuni ya 137 ya kanuni za kudumu za bunge ina complement ibara ya 84 (7) (d) ya Katiba" amesema Msigwa.


Mbunge huyo ni mmoja kati ya wabunge wa upinzani ambao wamekuwa wakilalamika Spika Ndugai kwa kudai kuwa analiendesha bunge kwa shinikizo na upendeleo, hivyo kudai kuwa hastahili kuendelea kuongoza kiti hicho.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search