Mechi Simba, Yanga Polisi watahadhalisha...soma habari kamili na Matukio360..#share

Na Salha Mohamed
 JESHI la Polisi Kanda maalum ya Dar es Salaam, linawataka mashabiki wasiokuwa na tiketi kutofika uwanjani ili kuepusha usumbufu watakaoupata katika mechi ya Ligi Kuu kati ya Simba na Yanga.

Kamanda wa Polisi, Lazaro Mambosasa
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Kamanda wa Kanda hiyo SACP, Lazaro Mambosasa amesema mechi hiyo inachezwa leo katika Uwanja wa Uhuru’ shamba la bibi’. ameahidi usalama wa kutosha katika mechi hiyo.

Amesema wananchi wasiwe na wasiwasi wa kiusalama na kupaswa kutoa ushirikiano kwa kutoa taarifa kwa jambo lolote watakaloliona kuwa linaweza kuwa chanzo cha uvunjifu wa amani kwa kipindi chote watakapokuwa ndani au nje ya uwanja.

“Mashabiki wanatakiwa kuwahi mapema ili kuepuka usumbufu unaoweza kutokea, tiketi hazitauzwa siku ya mechi hivyo mashabiki wanatakiwa kukata tiketi mapema,”amesema.

Amesema tiketi 23,000 zitauzwa kutokana na uwezo wa uwanja huo, hivyo kwa wale mashabiki watakaochelewa kukata tiketi wanashauriwa kuangalia mechi hiyo kupitia Television na kusikiliza Radio.

Amesema mashabiki wa pande zote mbili wanatakiwa kukaa katika sehemu zao maalumu watakazopangiwa huku akibainisha uwepo wa askari wa kutosha ili kuhakikisha sehemu zote za mageti ya kuingilia watu wanapekuliwa na magari hayataruhusiwa kuingia ndani ya uwanja bali watu wanatakiwa kuyapaki nje ya uwanja.


“Pamoja na hayo wananchi wanatakiwa kuwa watulivu katika kushangilia mechi hiyo, na kuepuka kuingia na chupa za maji, kuingia na mabegi, kuingia na silaha ya aina yoyote, kupaki magari ndani ya uwanja kukaa sehemu ambazo tiketi zao haziwaruhusu,”amesema Mambosasa.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search