Zitto kujibu mapigo kwa rais Magufuli..soma habari kamili na Matukio360..#share

Na Mwandishi wetu
 CHAMA cha ACT Wazalendo leo kinatarajia kutoa hadharani taarifa ya kamati kuu ya chama hicho kuhusu Takwimu za pato la taifa.

Kiongozi mkuu wa ACT Wazalendo, Zitto Kabwe
Takwimu hizo zitatangazwa  na kiongozi mkuu wa ACT Wazalendo, Zitto Kabwe ambaye pia ni mbunge wa Kigoma mjini

 Afisa habari wa ACT Wazalendo Abdallah Khamis amesema ‘Leo Oktoba 28, 2017, Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo, ndugu Zitto Kabwe atazungumza na Waandishi wa Habari kuhusu Taarifa ya Kamati Kuu ya Chama juu ya Takwimu za Pato la Taifa.’

Hatua hiyo inaaelezwa kuwa ni kujibu mapigo kwa rais Dk John Magufuli ambaye hivi karibuni alipokuwa akiwatunuku tuzo ya shukran wajumbe wa kamati za madini ya almasi, dhahabu na Tanzanite.

Katika hafla hiyo rais Magufuli alimtaka waziri wa Katiba Profesa Paramangamba Kabudi kuhakikisha sheria ya Takwimu inafanya kazi ili kudhibiti na kuwachukulia hatua za kisheria wote wanaotoa takwimu ambazo si sahihi.

Sheria hiyo inaelekeza yoyote atayekutwa na hatia ya kutoa Takwimu ambazo si sahihi afungwe miaka miwili

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search