NECTA yaonya udanganyifu mtihani kidato cha nne...Soma habari kamili na Matukio360...#share

Na Abraham Ntambara

WAKATI kesho wanafunzi  wa kidato cha nne wakitarajia kuanza mtihani wa kumaliza kidato cha nne, Baraza la Mtihani nchini (NECTA) limesema halitosita kumchukulia   hatua mwanafunzi yeyote pamoja wasimizi wa mitihani hiyo ambao watajihusisha na vitendo vya udanganyifu.
Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani nchini (NECTA), Dk. Charles Msonde

Pia, Baraza hilo  limewapa onyo wamiliki wa shule kuacha  kuwaingilia wasimamizi wa mitihani hiyo kwakuwa shule zao ni vituo maalum vya kufanyia mtihani.

Onyo hilo limetolewa leo Jijini Dar es Salaam, Katibu Mtendaji wa (NECTA), Dk. Charles Msonde wakati wa mkutano na waandishi,amesema Baraza hilo linatoa wito kwa  kwa wasimamizi wa mitihani  wote kufanya kazi yao kwa umakini na uadilifu.

“Tunawaasa wasimamizi wa mitihani pamoja na wanafunzi kujiepesha na vitendo vya udanganyifu  kwani Baraza  litachukua  hatua kali kwa yeyote  yule atakayebainika kukiuka taratibu za uendeshaji wa mitihani ya Taifa” amesema Dk Msonde.

Amesema Baraza hilo linawataka  wamiliki wa shule kutambua  kuwa shule zao ni vituo maalum vya mitihani  na hivyo havitakiwi kuingilia majukumu ya wasimamizi.

“Baraza halitasita kukifuta kituo  chochote cha Mitihani endapo litajiridhisha kuwa uwepo wake wa unahatarisha Usalama wa Mitihani ya Taifa”amesema Dk. Msonde.

Hata hivyo, Dk amesema Baraza hilo linaamini  kuwa walimu wamewaandaa vizuri wanafunzi hao kwa kipindi cha miaka mine ya elimu ya sekondari hivyo hakutakuwepo na vitendo vya udanganyifu.

Pamoja na hayo,Amesema katika mitihani huo Jumla ya watahiniwa 585,938 wamesajiliwa kufanya mtihani wa huo, ambapo kati yao watahiniwa wa shule ni 323,513 na watahiniwa wa kutegemea ni 62,425.

“Kati ya watahiniwa wa shule 323,513 waliosajiliwa ,wanaume ni 159.103 sawa na asilimia  49.18 na wanawake  ni 164,410 sawa na asilimia 50.82,huku watahiniwa wenye uono hafifu ni 305 ambapo maandishi yao yanakuzwa”amesema Dk. Msonde.

Kuhusu watahiniwa wa kujitegemea waliosajiliwa ni 62,425 ,wanaume ni 28,574 sawa na asilimia 45.77  na wanawake ni 33,851 sawa na asilimia 54.23 huku watahiniwa 6 wasioona.


Aidha,Baraza hilo linatoa wito kwa jamii kutoa ushirikiano katika kuhakikisha mitihani hiyo ambayo inaanza kesho octoba 30 hadi 17  Novemba 2017 inafanyika kwa Amani na Utulivu huku akiwaomba wananchi hao kuheshemu eneo la mtihani linapofanyika.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search