UTAFITI: Uwekezaji baharini chanzo samaki kuadimika...soma habari kamili na Matukio360..#share

Na Mwandishi wetu
WAKATI Tanzania ikikabiliwa na uhaba wa kitowewo cha samaki kwa siku za karibuni utafiti umeonesha  uwekezaji katika bahari kama kutafuta mafuta na gesi ni shughuli zinazochochea samaki kupotea au kwenda kwenye kina kirefu.
Mhadhiri wa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam Idara ya Sayansi za Maji na Uvuvi,Dk Benaisha Benno

Pia asilimia 90 ya wavuvi nchini kutumia zana duni hali inayopelea kuvua samaki tani 52,000 kwa mwaka ambao ni kidogo tofauti na rasilimali zilizopo kwenye bahari ya Hindi.

Hayo yamesemwa na mhadhiri wa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam Idara ya Sayansi za Maji na Uvuvi,Dk Benaisha Benno alipokuwa akitoa mafunzo kwa waandishi wa habari juu ya uharibifu wa mazingira kwenye bahari uliondaliwa na Shirika la Uhifadhi wa Mazingira la Umoja wa Mataifa (WWF).

"Bahari kwa sasa inakutana na changamoto nyingi kama uharibifu wa matumbao, kukata mikoko na kutafuta mafuta na gesi hali ambayo inakimbiza samaki katika kina kifupi na kwenda kina kirefu," amesema Dk Benno.

Benno amesema wavuvi hao hawana vifaa vya kisasa vitakavyowasaidia kuvua samaki katika bahari kuu matokeo yake wanashindwa kuvua samaki wakubwa na wengi ili waweze kujipatia kipato cha kuendeshea maisha yao.

Amesema sekta ya uvuvi ikitumika kikamilifu itakuwa na mchango mkubwa kwa uchumi wa nchi na wananchi.

"Tafiti ambayo ilifanyika 2014 inaonesha asilimia 90 ya wavuvi wanatumia dhana duni hali ambayo inasababisha washindwe kwenda kwenye kina kifupi hivyo wanapata samaki wachache," amesema.

Dk. Benno alisema kutokana na dhana duni wavuvi wameshindwa kuvua katika kina kirefu ambacho ni mita 200 hivyo wanakosa samaki wakubwa kama jodari.

Amesema ni wakati muafaka kwa serikali kuwekeza katika sekta hiyo ili kuhakikisha rasilimali zilizopo baharini zinatumika kwa usahihi.

Kwa upande wake Mtafiti Mwandamizi wa Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Tazania(Tafiri),Baraka Kuguru amesema sekta ya uvuvi ikipewa kipaumbele itachangia ukuaji wa uchumi na hivyo kutekeleza malengo ya viwanda na uchumi wa kati.

Kuguru amesema tafiti ziaonyesha kuwa sekta ya uvuvi imekuwa na mchango mkubwa kwa nchi ambazo zimewekeza hasa katika ukanda wa bahari ambapo rasilimali zilizopo kwenye bahari zina thamani ya dola za Marekani 333 bilioni huku uwekezaji ukiwa asilimia 20 mpaka sasa.

Dk Kuguru amesema pamoja na wavuvi kuwa na vifaa duni vya kuvulia ipo changamoto nyingine ya kuharibu mazalia ya samaki kama matumbao na mikoko hali ambayo inaweza kuchochea uvuaji samaki kupungua.

Akizungumza katika mafunzo hayo Meneja Kampeni ya kulinda Hifadhi ya Selous kutoka WWF, Atilio Tegalile alitoa rai kwa wanahabari kujikita katika habari za mazingira na bahari ili kuweza kusaidia nchi na wananchi hasa wanaojihusisha na uvuvi.
Meneja huyo amesema iwapo kutakuwa na kundi la wanahabari waliojikita kuandika habari za utunzaji mazingira na rasilimali za habari kutakuwa na mabadiliko chanya hivyo dhana ya uchumi wa viwanda itatekelezeka kirahisi.

"Natumia nafasi hii kuwaomba mjikite katika uandishi wa aina moja (specialization) kwani ndio uandishi wa sasa na mtapata tuzo, " amesema.

Mmoja wa wavuvi wa soko kuu la samaki la Zanzibar, Hamisi Arafat Hamisi ameiomba serikali iwatengenezee mazingira bora yatakayowawezesha kupata mikopo ili waweze  kununua vifaa vya kisasa vitavyoweza kufika bahari kuu ambapo wataweza kuvua samaki aina ya jodari na papa.

Kwa upande wake Mvuvi Omary Hamis amesema changamoto iliyopo ni  ukosefu wa boti yenye uwezo wa kuvua katika kina kirefu hali inayosababisha kuvua samaki wadogo na wachache.

"Boti tunazotumia zinaweza kuvua mita isiyozidi 30 hivyo kupelekea kupata samaki wachache na wadogo,tunaiomba Serikali isifikilie kuchukua kodi ijikite kwenye uwekezaji wa sekta ya uvuvi kwani ina faida kwa nchi na wananchi,alisema Hamisi.

            

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search