Polisi: Tunamshikilia Kigaila Benson wa Chadema..Soma habari kamili na Matukio360


Na Salha Mohamed

JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, limemshikilia Mkurugenzi wa Operesheni na Mafunzo(Chadema), Kigaila Benson kwa madai ya kutoa lugha za uchochezi na za kashfa.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam SACP Lazaro Mambosasa.

Kamanda wa Polisi wa Kanda hiyo, SACP Lazaro Mambosasa amethibitisha kukamatwa kwa Mkurugenzi huyo kwa mahojiano kwa madai ya kutoa lugha za kuikashfu serikali na watu wake.

Amesema"Tunaendelea kumshikilia na anaendelea kuhijiwa atakapokamilisha yale ambayo anamuhusu tutaelekeza kesi mahakamani kama ushahidi utakuwepo wa kutosha,"amesema.

Mambosasa amesema endapo ushahidi utakuwa wa kuendelea na mashahidi wengine wataangalia kupata dhamana huko mbele kwani jeshi hilo halijakamilisha yale waliokusudia.


"Tunaendelea na upelelezi na tukimaliza tutalileta kwenu kuwaambia hatua gani tumezichukua,"amesema.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search