Polisi wamkamata Zitto Kabwe...soma habari kamili na Matukio360..#share

Na mwandishi wetu
KIONGOZI mkuu wa chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe amekamatwa na Jeshi la Polisi.


Zitto Kabwe
Amekamatwa leo majira ya asubuhi  nyumbani kwake Masaki jijini Dar es Salaam

Afisa habari wa ACT Wazalendo, Abdallah Khamis ameiambia Matukio360 kuwa sababu za kukamatwa kwake ni hotuba aliyoitoa juzi katika mkuatano wake wa hadhara wa kampeni wa kumnadi mgombea udiwani kata ya Kijichi wilayani Temeke.

“Kiongozi wetu wa ACT Wazalendo Zitto Kabwe amekamatwa na Jeshi la Polisi muda huu(majira ya saa moja asubuhi) akiwa nyumbani kwake na amepelekwa kituo cha Polisi Chang’ombe.

“Sababu za kukamatwa kwake ni hotuba ya juzi(Jumapili) katika kata ya Kijichi,” amesema Khamis

Katika mkutano wa kijichi wa kumnadi mgombea udiwani wa ACT Wazalendo, Edga Mkosamali pamoja na mambo mengine Zitto alisema serikali inapika takwimu za ukuaji wa pato la taifa(DGP) na si sahihi kama ambavyo taasisi za serikali  zinavyotangaza.

Alisema Mkaguzi wa Hesabu za Serikali(CAG), anapaswa kufanya ukaguzi wa mapato ya serikali kwa Julai na Agosti mwaka  huu na kuiweka wazi kwa umma.

Zitto ambaye pia ni mbunge wa Kigoma mjini alisema mbali na CAG kufanya ukaguzi pia Mamlaka ya Mapato (TRA) ieleze mapato yake kwa kila idara pamoja na kuonesha marejesho na madeni yatakayokusanywa kama mapato.

Pia alizitaka Jumuia za Afrika Mashariki, Benki ya Maendeleo ya Afrika na Benki ya Dunia kufanya uchunguzi maalumu wa takwimu za uchumi nchini na kwamba hatua kali zichukuliwe dhidi ya serikali ya awamu ya tano ikigundulika kuwa takwimu juu ya ukuaji wa pato la taifa zimepikwa.


Kampeni za uchaguzi mdogo wa marudio wa udiwani utafanyika Novemba 26, 2017, utahusisha kata 43 nchini, Dar es salaam ikihusisha kata ya Mbweni, Kijichi na Saranga

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search