SIDO: Wajasiliamali boresheni bidhaa ...soma habari kamili na Matukio360..#share

 Na Salha Mohamed
SHIRIKA la kuhudumia viwanda vidogo(SIDO), limewataka wajasiliamali wadogo kujiimarisha na kufunga bidhaa zao kwenye vifungashio na kuweka lebo sahihi.

Anna Matinde kushoto akimsikiliza mmoja wa wajasiliamali 

Attachments area
Akizungumza na Matukio360 wakati wa kufunga maonesho ya wajasiliamali ya wakinamama jijini Dar es Salaam, Ofisa Masoko SIDO, Antonia Masoi amesema wajasiliamali wengi wamekuwa na changamoto ya vifungashio.

Amesema wajasiliamali wamekuwa na bidhaa nzuri lakini kinachowakwamisha ni kutokuwa na vifungashio vizuri na lebo sahihi.

“Bidhaa zao ni nzuri lakini wanatakiwa kuwa wakweli kwenye lebo zao itasaidia kujenga Tanzania ya viwanda,”amesema.

Amesema maonesho hayo yamekuwa na watu wachache waliofika kununua na kuangalia bidhaa kutokana na changamoto ya mvua iliyonyesha siku mbili zilizopita.

“Mvua imewaathiri watu kuja kuona, wengine waliona uvivu kuja kutokana na mvua kunyesha lakini hayakutangazwa tutajitahidi kutoa elimu ili washiriki zaidi kwenye maonesho,”amesema.
Rais wa Taasisi ya Uwezeshaji Wanawake Viccoba(Taswe), Anna Matinde amesema  wajasiliamali wadogo wanapaswa kuwa karibu na SIDO ili kukuza biashara zao.

Amesema kupitia maonesho hayo wajasiliamali wameweza kuwasiliana na kubadilishana mawazo katika biashara zao.

Amesema wapo waliojitahidi kuwa wabunifu katika kutengeneza lebo pamoja na kunadi biashara zao kupitia simu za mkononi.

“Kabla hujaingiza bidhaa sokoni angalia lebo uliyoweka inavutia? Wengine wanaweka majina ambayo si mazuri .

“Licha ya kuwa na mvua lakini haikuwavunja moyo …nimefurahishwa mmejifunza na hicho ndicho kilihowaleta si tuu kuuza bidhaa,”amesema.

Amesema serikali iko mbioni kutenga maeneo ya usindikaji bidhaa zenye ubora zikithibitishwa na Shirika la Viwango (TBS) na Mamlaka ya Chakula na Dawa(TFDA).

Amesema wajasiliamali wadogo hawataweza kuuza bidhaa zao kama hazitakuwa na TBS na TFDA pamoja na kufungasha kwenye vifungahio visivyo na ubora.

Matinde amesema wajasiliamali wanapaswa kuweka rekodi za mauzo na manunuzi ya kila mwezi huku akiitaka SIDO kuandaa mafunzo ya mahesabu kwa wajasiliamali hao.

Kauli mbiu ya maonesho hayo ni ‘Mwanamke mjasiliamali funguka shiriki Tanzania ya viwanda' ambapo maonesho hayo yanatarajiwa kufanyika mkoani Dodoma mwakani.





About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search