Serikali yanunua vifaa tiba vya Saratani...Soma habari kamili na Matukio360..#share

Na Salha Mohamed

SERIKALI imenunu vifaa tiba 100 vya tiba mgando ya mabadiliko ya awali ya saratani ya shingo ya kizazi (cryotheraapy) huku Tanzania ikiwa kinara wa ugonjwa huo Afrika.
Baadhi ya washiriki wakisikiliza kufungwa kwa mradi huo.

Hayo yamebainishwa leo wakati wa kufungwa kwa mradi wa uchunguzi na matibabu ya awali ya saratani ya mlango wa shingo ya kizazi uliofanyika miaka mitano kwa ushirikiano wa Chama cha Wazazi na Walezi (UMATI), PSI na Marie Stopes kwa uwezeshwaji wa taasisi ya Bill and Gates.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Msaidizi Kitengo cha Mama na Mtoto kutoka Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto, Dk Safina Yuna amesema mradi huo umesaidia kuboresha upatikanaji wa mabadiliko ya saratani ya mlango wa shingo ya kizazi katika vituo 90.

"Kama mnavyojua Tanzania inaongoza kwa saratani ya mlango wa kizazi hawa wametusaidia, Serikali imeamua kupanua wigo na kupunguza gharama za matibabu kwa wagonjwa."amesema.

Amesema takwimu zinaonesha wagonjwa wengi hufika hospitali ya Ocean road wakiwa katika hatua za mwisho ambapo matokeo ya matibabu yanakuwa si mazuri na kwamba  mgonjwa akiwahi hupona.

Amesema vifaa tiba hivyo vitatumika kutibu matibabu ya awali na upasuaji mdogo kwa wagonjwa wenye mabadiliko makubwa. Tayari vimeshasambazwa katika vituo 466 nchini .
"Tutatanua zaidi kuhakikisha huduma zinawafikia walengwa wengi ambao hawawezi kufika katika hospitali za wilaya na Mikoa pamoja na vituo vya afya nchini."

Mkurugenzi wa Mifumo ya Afya ya Marie Stopes, Jeremia Makula amesema mradi huo umefika katika mikoa 22 nchini.
"Katika kipindi cha maiaka 5  tumewafikia wanawake 187,267 katika uchunguzi wa saratani ya mlango wa shingo ya kizazi na tumegundua asilimia 4.2 walikuwa na mabadiliko ya awali ya kansa ya kizazi,"amesema.

Ameongeza kuwa wametibu wanawake 7600 sawa na asilimia 100 ya waliokuwa wakihitaji matibabu ya awali ya mabadiliko ya awali ya saratani ya mlango wa shingo ya kizazi.

Amesema wanawake 1000 wamekuwa wakihitaji huduma ya juu huduma ambapo walipewa rufaa ya matibabu katika hospitali zinazotoa huduma hiyo.

Makula amesema katika mradi huo wameanza kutumia kipimo kipya ambacho hakijawahi kutumika hapa nchini licha ya kuwa na changamoto nyingi katika kuwafikia waliokuwa vijijini.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search