Polisi Dar wamshikilia Sheikh Issa Ponda..Soma habari kamili na Matukio360..#share

JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linamshikilia Sheikh Issa Ponda kwa tuhuma za uchochezi.
 Sheikh Issa Ponda

Kukamatwa huko ni baada ya Sheikh Ponda akiwa na mawakili wake  leo kujisalimisha katika kituo cha kikuu cha kati cha Polisi kutii agizo lililotolewa hivi karibuni na mkuu wa polisi kanda maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa.

Wakili wa Sheikh Ponda, Profesa Abdallah Safari ameiambia Matukio360 kuwa hadi sasa Polisi wanamshilia Sheikh Ponda  na kwamba dhamana ipo wazi.

Polisi wametaka watu watatu wa kumuwekea dhamana Sheikh Ponda, mmoja wapo lazima awe mtumishi wa serikali.

Hivyo hadi muda huu tumeshapata wadhamini wawili bado mmoja hivyo muda wowote ataachiwa kwa dhamana.

Profesa Safari ambaye pia ni makamu mwenyekiti wa CHADEMA amesema Sheikh Ponda anashikiliwa kwa tuhuma za uchochezi.

pamoja na mambo mengine Ponda anashikiliwa
Hivi karibuni Sheikh Ponda alitoa taarifa mbalimbali kutokana na matukio yanayoendelea ikiwamo mwenendo mzima wa mauaji, maiti kuokotwa, raia na viongozi kadhaa kutekwa na kupotea

 Katika mkutano wake na waandishi wa habari  Sheikh Ponda alisema Watanzania wamekata tamaa na usalama wao  na wanaishi kwa hofu na kwamba kama Serikali inawajibika ipasavyo matukio hayo yasingekuwepo.

‘’Serikali imekuwa ikiwaandama baadhi ya viongozi wa dini na wa vyama vya siasa hasa vya upinzani, wakati  viongozi hao ndiyo wanaoikumbusha serikali wajibu wake na sasa  wamekuwa wakifikwa na hatari ikiwamo kupata vilema vya kudumu.’’ Na kuongeza ‘’Mimi binafsi nilipigwa risasi hadharani mwaka 2013  na hivi sasa Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) Tundu Lissu .’’

Sheikh Ponda aliiomba Serikali kuacha kuwazuia viongozi wa upinzani kuzungumza mambo mbalimbali yahusuyo nchi.

‘’Serikali imezuia haki za kidemokrasia kwa viongozi wa upinzani. Imezuia kufanya mikutano ya hadhara na maandamano ya amani.’’

                                                                                                              

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search