Sheikh Ponda awatoroka Polisi kikomando...Waandishi watatu wakamatwa ..#share
NI kama Filamu, Hivyo ndivyo unavyoweza kusema kufuatia
Sheikh Issa Ponda kuwatoroka askari polisi zaidi ya kumi waliotaka
kumkamata.
Sheikh Issa Ponda akizungumza na waandishi wa habari
Tukio hilo limetokea leo majira
ya saa tano asubuhi jijini Dar es Salaam katika hoteli ya Iris baada
ya askari polisi kuvamia katika mkutano wa waandishi ambapo Sheikh
Ponda alikuwa akitoa taarifa mbalimbali kutokana na matukio yanayoendelea ikiwamo
mwenendo mzima wa mauaji, maiti kuokotwa, raia na viongozi kadhaa kutekwa na
kupotea.
‘’Inaonekana baadhi ya askari
polisi hawamfahamu sheikh Ponda kwani amewapita hapa wakiwa
wanarandaranda na kutoka nje na kutokemea upande wa kulia wa hotel ya Iris.’’
Shuhuda amesema Sheikh Ponda
alipishana na baadhi ya askari wanne ambao ndio wanaomjua vizuri kwa yeye
kutumia njia ya miguu (ngazi) huku askari
kanzu wakitumia lifti
hotelini hapo.
Awali katika mkutano huo, Sheik
Ponda alisema Watanzania wamekata tamaa na usalama wao na wanaishi
kwa hofu na kwamba kama Serikali inawajibika ipasavyo matukio hayo
yasingekuwepo.
‘’Serikali imekuwa ikiwaandama
baadhi ya viongozi wa dini na wa vyama vya siasa hasa vya upinzani,
wakati viongozi hao ndiyo wanaoikumbusha serikali wajibu wake na
sasa wamekuwa wakifikwa na hatari ikiwamo kupata vilema vya
kudumu.’’ Na kuongeza ‘’Mimi binafsi nilipigwa risasi hadharani mwaka
2013 na hivi sasa Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS)
Tundu Lissu .’’
Pia Sheikh Ponda ameiomba
Serikali kuacha kuwazuia viongozi wa upinzani kuzungumza mambo mbalimbali
yahusuyo nchi.
‘’Serikali imezuia haki za
kidemokrasia kwa viongozi wa upinzani. Imezuia kufanya mikutano ya hadhara na
maandamano ya amani.’’
Awali Polisi walifika
hotelini hapo wakiwa na gari mbili aina ya Defender wakiwa na silaha za moto
kwa lengo la kumkamata Sheikh Ponda na kumzuia asizungumze na waandishi wa
habari.
Wakati huo
huo, waandishi watatu kutoka vyombo mbalimbali vya
habari walikamatwa na polisi hao na kupakiwa garini
na kupelekwa mahala kusikojulikana.
Kukamatwa kwao kulitokana na
hatua yao ya kuwapiga picha polisi na gari zao na pia kuangali
kilichozungumzwa na Sheikh Ponda.
Hata hivyo wakati tunarusha
habari hii, waandishi hao waliachiwa huru baada ya kushikiriwa
kwa saa tatu
No comments:
Post a Comment