Tundu Lissu ampa ujumbe maalum Sheikh Ponda..Soma Habari Kamili na Matukio360..#share


SHEIKH Issa Ponda amesema Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Tundu Lissu ameahidi kuendelea na harakati za ukombozi na kupigwa kwake risasi kumemuongezea ujasiri zaidi.
Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu

Ponda ameyasema hayo leo katika mkutano wake na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam na kwamba afya ya Lissu inaendelea kuimarika.

‘’Hivi karibuni nilikuwa nchini Kenya alikolazwa Lissu kumjulia hali yake, kumuombea dua na kumjengea matumaini ya afya yake na matumaini endelevu ya harakati zake za umma na kujenga mazingira ya kutosha ili niweze kuzungumzia  ipasavyo matukio ya mauaji, kuokotwa kwa maiti na kubanwa kwa uhuru wa viongozi na raia kuzungumza na kukemea maovu .’’

Amesema  walizungumza vya kutosha na kwamba Lissu ameahidi pindi atakaporejea nchini ataendeleza mapambano na kamwe hawezi kukaa kimya.

‘’Amenieleza kazi muhimu anazofanya akiwa pale kitandani huku akiamini damu yake na yangu na zingine zitakazomwagika kwa namna hii zitawalipa watanzania kwa kupata uhuru wa kweli wenye thamani.’’ amesema

Sheikh Ponda amesema amehimizwa na Lissu mshikamano huku akiwa na matumaini ya kuwepo watu kama yeye wenye fikra na matumaini ya kuifikisha nchi sehemu salama.
Amesisitiza na kuwataka  Watanzania  kuwa na nguvu ya pamoja katika kutetea maslahi ya taifa.

‘’Wanaoamini hali iliyopo sasa inatokana na serikali kushindwa kutekeleza wajibu wake tuunganishe nguvu kuhakikisha serikali inatekeleza wajibu wake.’’

Sheikh Ponda amewataka viongozi wa dini, wasomi, viongozi wa vyama vya upinzani na viongozi  wa CCM waiambie Serikali ukweli.

Kimya chao ni hasara na kitawanyima hadhi na kwamba kuonyesha hisia wazi ni jambo muhimu katika maisha.




About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search