Sitta Awataka Wenyeviti na Watendaji wa Serikali za Mitaa Kuwa Waadilifu..Soma Habari Kamili na Matukio360..#share

Na Mwandishi Wetu

MEYA wa Manispaa ya  Kinondoni   Benjamini Sitta  amewakata wenyeviti  na watendaji wa mitaa  kuwa waadilifu na  wabunifu  katika sehemu zao za kazi ili kupunguza kero  za wanachi.

Meya wa Kinondoni Benjamini Sitta akizungumza wakati wa ufunguzi wa semina ya watendaji na wenyeviti  wa Serikali za Mitaa jijini Dar es Salaam Leo.

Sitta amesema hayo leo wakati akifungua semina ya watendaji na wenyeviti  hao ambayo imeratibiwa na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam yenye lengo la kuwajengea uwezo katika utekelezaji wa majukumu yao katika kuwatumikia wananchi, na amewataka kubadililika kuendana na wakati uliopo katika utoaji wa huduma.

Amewataka kutokuwa na vinyongo  wakati mambo yanapokuwa yameamriwa   bali kutoa maoni yao kwa Manispaa ili kuboresha utendaji kazi na kuleta maendeleo katika manispaa hiyo.

Aidha, amesema kuwa utaratibu wa kutuma barua  kwa mkono  umepitwa na wakati , na kwamba  utaratibu  wa kutumia  mfumo wa kisasa unaandaliwa  ili kurahisisha utoaji huduma kwa wanachi. 

Ameongeza  kuwa Manispaa hiyo inakabiliwa na migogoro mingi ya ardhi kuliko sehemu yoyote Tanzania  huku akibainisha  kuwa  baadhi yao wamechangia tatizo hilo, na kuwataka kuainisha maeneo yote yasiyoendelezwa kwa muda mrefu na maeneo   ambayo  hayajapimwa pamoja na maeneo  ya uwekezaji.
Nao baadhi ya wenyeviti wa  na watendaji wa mitaa waliohudhuria semina hiyo wamesema  kumekuwa na changamoto kubwa ya njia nabarabara katika maeneo yasiyo pimwa  na yamekuwa yakisababisha shida kubwa  na ufinyu wa njia kubanana kwa mitaa  na kusababisha maeneo mengi kuwa machafu kwa sababu ya baadhi ya wananchi  kutochangia gharama za usafi wa uzoaji taka.

“kumekuwa pia na wafanyabiashara ndogo  hawa wamachinga  wanakaidi maelekezo wanapanga bidhaa zao hadi barabarani hapa  maeneo ya kwa  Ndevu Tegeta  kwa  kisingizio kuwa Rais amewaruhusu kufanya biashara na wengine wamejenga vibanda katika mtaro wa TANRODS,  kwa kweli  hili na ni kero na halikubaliki kabisa  lazima waheshimu  miundombinu na tutawahamisha ‘’ . Amesema Luteni Kanali  Mstaafu wa Mtaa wa Tegeta  Ahaba  Lwiva .

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search