TAARIFA KWA UMMA KUHUSU FISI ALIYEUAWA KITUO CHA MABASI CHA UBUNGO-DAR ES SALAAM..
Tarehe 23/09/2017 ilitolewa taarifa katika mitandao ya kijamii kuwa mnyamapori (fisi) aliua katika kituo cha mabasi ubungo, Dar es Salaam. Taarifa hiyo iliambatana na picha ya video video clip inayoonyesha watu waliovaa mipira ya mikononi Gloves na wengine wengi wakiangalia fisi mmoja aliyekuwa amelala chini akionekana amekufa. Taarifa zilisema askari wa usalama barabarani wa kituo hicho cha mabasi walimpiga risasi mnyama huyo.
Kufuatia taarifa hiyo, Mamlaka ya Usimamizi wanyamapori Tanzania (TAWA) tulifuatilia na kubaini kuwa hakuna fisi wala mnyamapori yeyote anayefanana naye aliyeuwa kituoni hapo tukathibitisha kuwa ni uzushi na uongo. Hatua tulizopitia kuthibitisha haya ni kama ifuatavyo:-
Hakuna taarifa ya tukio katika vituo vya polisi na Ofisi ya Manispaa ya Jiji inayosimamia uendeshaji wa huduma katika kituo hicho
Hakuna majengo katika kituo hicho wala jirani yanayofanana na yale yanayoonekana katika clip hiyo
Kutokana na mahusiano mazuri kati ya TAWA na vyombo vingine vya usalama, tungeitwa kushiriki kumthibiti mnyama huyo kama angetokea kuwepo
Tunaomba Umma upuuze taarifa hiyo kwani siyo ya kweli.
Limetolewa
Na
KAIMU MKURUGENZI MKUU-TAWA
Kufuatia taarifa hiyo, Mamlaka ya Usimamizi wanyamapori Tanzania (TAWA) tulifuatilia na kubaini kuwa hakuna fisi wala mnyamapori yeyote anayefanana naye aliyeuwa kituoni hapo tukathibitisha kuwa ni uzushi na uongo. Hatua tulizopitia kuthibitisha haya ni kama ifuatavyo:-
Hakuna taarifa ya tukio katika vituo vya polisi na Ofisi ya Manispaa ya Jiji inayosimamia uendeshaji wa huduma katika kituo hicho
Hakuna majengo katika kituo hicho wala jirani yanayofanana na yale yanayoonekana katika clip hiyo
Kutokana na mahusiano mazuri kati ya TAWA na vyombo vingine vya usalama, tungeitwa kushiriki kumthibiti mnyama huyo kama angetokea kuwepo
Tunaomba Umma upuuze taarifa hiyo kwani siyo ya kweli.
Limetolewa
Na
KAIMU MKURUGENZI MKUU-TAWA
No comments:
Post a Comment