Tanesco Walia na Vishoka, 116 Wadakwa Wakitumia Umeme Bure..Soma Habari Kamili na Matukio360..#share

Na Salha Mohamed

SHIRIKA la Umeme nchini (Tanesco), limepata hasara zaidi ya Sh. Mil 116 kwenye operesheni ya kukagua mita za umeme kwa wakazi wa Mkoa wa Dar es Salaam huku wateja 116 wakikamatwa  kwa kutumia umeme bure.
Fundi Umeme wa shirika la Tanesco, Zuberi Kediga, akiwa juu ya moja ya nyumba ya Mteja maeneo ya Tegeta akikata waya wa umeme baada ya kubaini kuiba umeme kinyume na sheria wakati wa Oparesheni inayoendelea jijini Dar es Salaam. Mteja huyo aliyekuwa akiiba umeme. Picha na Prona Mumwi 

Operesheni hiyo endelevu imeanza Septemba 26 mwaka huu, imewafikia wananchi 5,444 ikiwa na lengo la kuangalia miundombinu ya Shirika hilo kwa Kanda ya Mkoa huo kwa kila mtumiaji wa umeme.

Akizungumza jana wakati wa Operesheni hiyo, Mhandisi Mkuu Mkaguzi na Udhibiti wa Mapato Kanda ya Dar es Salaam na Pwani, Mrisho Sangiwa amesema kati ya watumiaji 5,444 wa umeme, mita 49 zimekutwa hazitumii umeme vizuri.

“Tumebadilisha mita zaidi ya 100. Tukiangalia mahesabu yaliyopatikana kwa wateja waliokuwa wanamatatizo ni zaidi ya sh. Mil 166 hadi leo(jana) na robo ya pesa hizo zimeshalipwa,”amesema.

Amesema Operesheni hiyo itafika kwa kila mtumiaji wa umeme mkoani humo na Pwani, ambapo mteja atakayekutwa akiiba umeme atachukuliwa hatua za kisheria kwani wizi wa umeme ni kosa kwa kuingilia miundombinu ya Shirika kwani sheria ya umeme ya 2008 imebainisha.

Mhandisi Sangiwa amesema wananchi wanapaswa kuepuka vishawishi vya vishoka kwa kuwaunganishia umeme bure kwani kunaweza kusababisha mlipuko na kuuunguza nyumba na kubainisha kuwa wakikamatwa gharama zake ni kubwa hivyo watumie umeme kulingana na matumizi yao.

 Amesema miundombinu ya umeme ni gharama wananchi wanapaswa kuipenda ili kulipa kodi serikalini kwa kulipa bili na hata kusaidia wananchi wasiokuwa na umeme kuunganishiwa nishati hiyo hadi vijijini.

Ameongeza kuwa kwa sasa wanaendelea kutoa elimu kwa wananchi  kwani  wengi hawana elimu ya matumizi sahihi ya vifaa vya  umeme na  matumizi yake, muda wa kifaa hicho(uchakavu) na si kuvilalamikia ubora wake.

“Wananchi tuungane kupiga vita wizi wa umeme, na huu mchakato ni endelevu,msishawishiwe na vishoka kwa kuwawekea umeme bure, vishoka ni mafundi umeme wengi hawajasajiliwa, wananchi wawe makini,”amesesma.

Ameongeza kuwa wapo vishoka wanaojifanya kukagua miundombinu ya umeme majumbani  kwa kuwatengenezea lakini bnaadae humwambia kishoka mwenzie na kujitambulisha kama ni ofisa kutoka Tanesco na kukagua ili kujipatia fedha.

Mhandisi Sangiwa amewataka wananchi kudai vitambulisho endapo atakuja mkaguzi wa kukagua miundombinu ya umeme ambapo kama mteja atakuwa na wasiwasi asisite kupiga simu Tanesco ili kuchukuliwa hatua.

Ametoa wito kwa wananchi kuwa wazalendo kwa kulinda miundombinu ya umeme  ili kutekeleza sera ya uchumi wa viwanda na kulijenga taifa na kutoa taarifa kwa wanaokiuka taratibu na sheria za shirika hilo kwa kupewa zawadi.



Fundi Umeme wa Shirika la Tanesco, Issaya Haule, akionesha waandishi wa habari  mita iliyochezewa na vishoka katika moja ya nyumba iliopo eneo la Tegeta mtaa wa Panga Dar es Salaam.

Mhandisi Mkuu Mkaguzi Udhibiti wa Mapato Kanda ya Dar es Salaam na Pwani, Mrisho sangiwa, (kushoto) akitoa maelezo kwa mafundi na maofisa wa Shirika la Tanesco kuhusu oparesheni ya ukaguzi wa mita.


Moja ya nyaya zilizounganishwa kwa wizi wa umeme

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search