TECNO kuja na Smartphone yenye ‘internal memory’ kubwa..Soma habari kamili na Matukio360..#share


ZILE zama ambazo ule ujumbe wa "hauna nafasi ya kuhifadhi vitu kwenye simu yako" ulikua unaboa sana kwenye smartphones zetu, zishapitwa na wakati. Hakika tumeona Tecno wakijaribu kutusaidia katika tatizo hilo kwa kutuletea simu ambazo zina uwezo mkubwa sana wa kuhifadhi vitu, yaani internal memory. Tuchukulie mfano simu ya Phantom 6 plus ambayo ina ukubwa wa 64GB kama internal memory. Hongereni sana Tecno katika hilo.


Tukizungumzia memory, tunaongelea vitu viwili, ROM na RAM. Kiufupi ROM ni ule ukubwa wa nafasi ya kuhifadhi vitu katika simu yako na RAM ni kitu inayowezesha simu yako ifanye kazi kwa uharaka bila ya kustack.

Tecno wamefanya kazi nzuri sana katika vitu hivyo viwili. Sasa basi kwakua Phantom nyingine ipo njiani inakuja, ni dhahiri kua tunategemea vitu vizuri na vikali zaidi. Phantom 6 plus ilikua kiboko, huku nina kitu cha 64GB ya ROM, kule nina 4GB za RAM, yaan ulikua ni mwendo wa kucheza magemu tu makubwamakubwa kwa kasi ya ajabu.


Hakika sitarajii kitu chochote pungufu katika huyo bwana mkubwa Phantom anayekuja. Nitafurahi sana kama Phantom inayokuja itakua na uwezo wa ROM sio chini ya 64GB, au hata kama wakiamua kunibariki na kitu cha 128GB itakua fresh. Tukija kwenye RAM palee..tafadhali tuleteeni 6GB hizo. Ebhana kama Phantom inayokuja itakua imebeba hiyo mizigo, lazma niitie mkononi.

Sasa kwa wale wote wachezaji magemu sana, hakika RAM itawatendea vyema sana. Na kwa wale wenzangu wa kuangalia mamuvy nini kwenye simu, internal storage kubwa hiyo itakuwezesha uhifadhi mamuvy kibao tu.

Basi wote tukae mkao wa kula… Kitu cha Phantom kinakuja.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search