Serikali kununua ‘vichwa’ vya Magufuli..soma habari kamili na Matukio360..#share
SERIKALI ya Tanzania inatarajia
kununua vichwa 15 vya treni ambavyo Rais Magufuli alivikuta
bandarini vikiwa havina mwenyewe mwanzoni mwa mwezi Julai, 2017. Pia imeunda
tume ya watu 11 kuvichunguza.
Vichwa vya treni vilivyopo Bandarini
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa amesema hayo leo jijini Dar es Salaam na kusema kuwa serikali imekusudia kuvinunua vichwa hivyo vya treni kwa matumizi endapo vitakuwa ni vizima na kama havitakuwa na matatizo yoyote.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa amesema hayo leo jijini Dar es Salaam na kusema kuwa serikali imekusudia kuvinunua vichwa hivyo vya treni kwa matumizi endapo vitakuwa ni vizima na kama havitakuwa na matatizo yoyote.
Prof. Mbarawa amesema endapo
vichwa hivyo vikionekana ni vizima kwa mujibu wa uchunguzi ukaofanywa na tume
hiyo ya watu 11 iliyoundwa na serikali hivyo serikali itakaa chini na mmiliki
wa vichwa hivyo 15 vya treni na kuzungumza naye biashara.
Mwezi Julai Rais Magufuli alipokuwa
akiweka jiwe la msingi katika mradi wa upanuzi wa Bandari ya Dar es Salaam
alisema ameviona vichwa vya treni zaidi ya 15 ambavyo kwa muda huo vilikuwa
vinaonekana havina mmiliki, na kudai kuwa vichwa hivyo vya treni ni vibovu.
Rais aliagiza Wizara husika kulifanyia kazi jambo hilo ili ukweli ufahamike
kuhusu vichwa hivyo 15 vya treni.




No comments:
Post a Comment