TMA yatabiri mvua kubwa.. yawataka wananchi kujihadhari.. soma taarifa kamili na matukio360.. #share
Na Salha Mohamed
MAMLAKA ya hali ya hewa nchini(TMA), imewatahadharisha wananchi kunyesha kwa mvua kubwa ndani ya saa 24.
Mvua hiyo iliyozidi milimita 50 inatarajiwa kunyesha kuanzia Oktoba 31 hadi Novemba 3, 2017.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na mamlaka hiyo leo, imesema kuwa kiwango cha mvua hiyo ni cha uhakika wa juu kwa asilimia 80.
Taarifa hiyo imeainisha baadhi ya maeneo yatakayoathirika zaidi kuwa Tanga, Dar es Salaam Pwani pamoja Visiwa vya Unguja na pemba.
Pia kuelekea Novemba 3 mwaka huu, mvua hiyo inatarajia kusambaa katika maeneo ya Mkoa wa Lindi
Hali hiyo ni kutokana na kuwepo na kuimarika kwa ukanda wa mvua (Inter tropical Convergency Zone-ITCZ) katika maeneo hayo.
Mamlaka hiyo imetoa tahadhari kwa wakazi wa maeneo yaliyotajwa na kuchukua tahadhari stahiki na kuendelea kufuatilia taarifa pamoja na tahadhari zilizotolewa huku ikiendelea kutoa mrejeo kila itakapobidi.
MAMLAKA ya hali ya hewa nchini(TMA), imewatahadharisha wananchi kunyesha kwa mvua kubwa ndani ya saa 24.
Mvua hiyo iliyozidi milimita 50 inatarajiwa kunyesha kuanzia Oktoba 31 hadi Novemba 3, 2017.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na mamlaka hiyo leo, imesema kuwa kiwango cha mvua hiyo ni cha uhakika wa juu kwa asilimia 80.
Taarifa hiyo imeainisha baadhi ya maeneo yatakayoathirika zaidi kuwa Tanga, Dar es Salaam Pwani pamoja Visiwa vya Unguja na pemba.
Pia kuelekea Novemba 3 mwaka huu, mvua hiyo inatarajia kusambaa katika maeneo ya Mkoa wa Lindi
Hali hiyo ni kutokana na kuwepo na kuimarika kwa ukanda wa mvua (Inter tropical Convergency Zone-ITCZ) katika maeneo hayo.
Mamlaka hiyo imetoa tahadhari kwa wakazi wa maeneo yaliyotajwa na kuchukua tahadhari stahiki na kuendelea kufuatilia taarifa pamoja na tahadhari zilizotolewa huku ikiendelea kutoa mrejeo kila itakapobidi.
No comments:
Post a Comment