Wabunge waibua hoja dhidi ya wateule wa JPM..Soma habari kamili na Matukio360..#share
Na Mwandishi Wetu
WABUNGE wameibua hoja ya nani ni kiongozi mkubwa kwa cheo kati ya wabunge, wakuu wa wilaya na mikoa .
WABUNGE wameibua hoja ya nani ni kiongozi mkubwa kwa cheo kati ya wabunge, wakuu wa wilaya na mikoa .
Wabunge wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.
Hoja hiyo imeibuka leo mjini Dodoma katika semina ya wabunge
wa kamati mbili za Bunge kuhusu masuala ya kidiplomasia na itifaki ambayo
imeandaliwa na Bunge kupitia Mradi wa
Kujengea Uwezo Wabunge na Wawakilishi unaofadhiliwa na Shirika la Umoja wa
Mataifa la Mpango wa Maendeleo (UNDP).
Aidha washiriki katika semina ni wajumbe wa Kamati ya Mambo
ya Nje, Ulinzi na Usalama; Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC) na wawakilishi
kutoka vyama vya kibunge.
Akichangia katika semina hiyo Mbunge wa Sumbawanga Mjini
(CCM), Aeshi Hillal ametoa mfano wa ziara za kikazi akisema mbunge huwekwa wa
mwisho, akitanguliwa na mkuu wa mkoa na mkuu wa wilaya.
“Unakuta mkoa katika ziara gari la mbele yupo RC ameweka
bendera, linalofuatia ni la DC naye ameweka bendera na la mbunge linakuwa
nyuma. Tunaomba utufafanulie katika hilo,” amesema.
Kwa upende wake Mbunge wa Morogoro Kusini-Mashariki (CCM),
Omary Mgumba amesema mkuu wa wilaya anamwakilisha Rais na katika wilaya
nyingine huwa zina majimbo mawili ya uchaguzi, hivyo kumfanya mbunge kuwa na
eneo dogo la kiutawala ikilinganishwa na mkuu wa wilaya.
“Siku zote ukweli ni mchungu na hasa ukiwa hutaki kuusikia.
Utakuta wilaya moja ina majimbo mawili, mbunge wa jimbo moja utawala wake ni
kwenye jimbo lake tu lakini mkuu wa wilaya ni mtawala katika majimbo yote
mawili yaliyo katika wilaya yake,” amesema.
Akizungumzia hilo, Mbunge wa Mtambile (CUF), Mosoud Abdallah, amehoji itifaki inazungumzaje kuhusu mbunge wa jimbo na wa viti maalumu wanapokuwa jimboni.
“Tunapokuwa jimboni ni mbunge gani anakuwa mkubwa kwa cheo kati ya mbunge wa viti maalumu na wa jimbo,” amehoji.
Akijibu hoja hizo, ofisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje, Kitengo cha Uhusiano wa Kimataifa, Ally Masabo amesema kiitifaki mkuu wa mkoa ndiye mwenye mamlaka katika mkoa, hivyo ndiye anayetakiwa kuwa mbele katika msafara mkoani.
"Suala hili wabunge wana wajibu wa kuangalia, na utatuzi upo kwenu wabunge," amesema Masabo ambaye ametoa mada katika semina hiyo.
Akizungumzia hilo, Mbunge wa Mtambile (CUF), Mosoud Abdallah, amehoji itifaki inazungumzaje kuhusu mbunge wa jimbo na wa viti maalumu wanapokuwa jimboni.
“Tunapokuwa jimboni ni mbunge gani anakuwa mkubwa kwa cheo kati ya mbunge wa viti maalumu na wa jimbo,” amehoji.
Akijibu hoja hizo, ofisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje, Kitengo cha Uhusiano wa Kimataifa, Ally Masabo amesema kiitifaki mkuu wa mkoa ndiye mwenye mamlaka katika mkoa, hivyo ndiye anayetakiwa kuwa mbele katika msafara mkoani.
"Suala hili wabunge wana wajibu wa kuangalia, na utatuzi upo kwenu wabunge," amesema Masabo ambaye ametoa mada katika semina hiyo.
No comments:
Post a Comment