Waziri Mpina apiga marufuku mnada wa mifugo...Soma habari kamili na Matukio360...#share

Na Mwandishi Wetu

WAZIRI wa Mifugo na Uvuvi Luhaga Mpina amepiga marufuku kupigwa mnada mifugo inayokamatwa kwenye hifadhi mbalimbali nchini bila maafisa mifugo kuipima na kujiridhisha kama haina magonjwa.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Luhaga Mpina

Marufuku hiyo ameipiga leo Wilayani Kasulu Mkoani Kigoma aliposhiriki katika zoezi la ukamataji wa mifugo Zaidi ya 170 iliyoingia kutoka nchi jirani ya Rwanda.

Amesema “ili kuepuka kuenea kwa magonjwa ya wanyama hao sambamba na kuwachukulia hatua kali wananchi ambao wamekuwa wakipokea na kubeba dhamana ya mifugo kutoka nje ya nchi huku wakidai kuwa ni ya kwao,”.

Aidha amebainisha kuwa kufanya hivyo ni kinyume cha sheria na amewataka wafugaji wanapokamatiwa mifugo yao wajitokeze mara moja ili kuepuka usumbufu unaojitokeza.

Waziri Mpina amesema serikali itaendelea kuwachukulia hatua kali wananchi ambao wamekuwa wakipokea na kukubali kubeba dhamana ya mifugo kutoka nje ya nchi huku wakidai kuwa ni ya kwao



About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search