Makonda amjibu waziri Lukuvi... soma habari kamili na Matukio360.. #share

Salha Mohamed
MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, amewatoa hofu wananchi mkoani humo kuwa haitavunja nyumba ya mtu na amewataka watoa vibali, kuvitoa ndani ya mwezi mmoja tangu kupokea maombi.


 Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda

Makonda ameyasema hayo kupitia waraka alioutoa kwa vyombo vya habari baada ya kile kinachodaiwa kufanyika kwa uvunjaji wa nyumba za wananchi wa karne.

Ameseeza  serikali inayoongozwa na Rais, Dk. John Magufuli haivunji nyumba ya mtu bali inaendelea kurasimisha makazi kama ambavyo ilifanya kwa
wakazi wa Kimara kwa kuwapatia hati wananchi 6000 waliokuwa wamejenga kwenye makazi yasiyo rasmi.

"Naomba niseme kwenye Mkoa wa Dar es Salaam hapatakuwa na bomoa bomoa ya karne wala nyumba ya mtu kuvunjwa, isipokuwa wananchi wanaojenga sasa ni vyema wakafuata utaratibu kama alivyoelekeza Waziri Lukuvi, ili kuepuka kuvunjiwa nyumba ambayo umeijenga kwa jasho jingi, na kujinyima huku ukikesha ili utimize ndoto ya kuwa na makazi bora,"amesema.


Amesema jitihada zinaendelea na ndivyo itakayofanyika Oktoba 27, 2017 kwa wananchi waliojenga katika maeneo ya makongo juu.

"Naomba kuwatoa hofu. Naomba niseme, na kama nimemuelewa vizuri alichokisema Waziri wa Ardhi, Nyumba na maendeleo ya Makazi, William Lukuvi wananchi wasiendelee kujenga bila vibali vya ujenzi jambo ambalo linawanyima haki yao ya kukopeshwa, kulipa kodi ya majengo, na mwishoni kuwa na miji isiyopangwa vizuri,"amesema.

Makonda amekiri kuwa hapo awali kulikuwa na changamoto ya upatikanaji wa vibali vya ujenzi jambo ambalo haliwezi kuwa adhabu kwa Wananchi waliojenga miaka ya nyuma.

Amesema "Ilifika hatua mwananchi ana Hati ya Kiwanja chake na amekamikisha michoro kwa mujibu wa Sheria na ana fedha za kuanza Ujenzi kwa ajili ya Makazi ya kuishi, Mwananchi huyo analazimika kufuatilia manispaa kwa zaidi ya miaka miwili hadi mitatu bila kupata kibali cha ujenzi.

"Na hata akipata kibali baada ya miaka mitatu na kuanza ujenzi, unakuta ndani ya muda mfupi watakuja baadhi ya watu wa OSHA kumsimamisha kwa madai hawana taarifa ya ujenzi jambo linalotengeneza mianya ya Rushwa,"amesema.

Amesema mwananchi huyo akimalizana na watu wa OSHA Wanakuja baadhi ya watu wa kikosi cha zimamoto (fire) jambo linalosababisha atafute utaratibu wa kumalizana nao, jambo linalokera wananchi na kuwafanya wakose hamasa ya Kutafuta vibali vya ujenzi na Hatimae kujenga kiholela.

Makonda ameongeza kuwa kutokana na jambo hilo, baadhi ya watu wasiowaaminifu wanatumia mwanya huo kuvamia maeneo ya watu na kujenga Kiholela na kuibua Migogoro Mikubwa ya Ardhi.

Kutokana na changamoto hizo, Serikali ya Mkoa imefanya kikao na wataalamu wa Ardhi ambapo vitengo vinanavyohusika na Utoaji wa vibali vya ujenzi vinapaswa kuwa na mfumo mmoja wa mawasiliano (one stop center) ili mwananchi atakapoomba kibali cha ujenzi Idara zote zifikiwe kwa wakati Mmoja na kupunguza usumbufu wa mwananchi kwenda kufuatilia vibali.

"Ili mfumo huo uanze kufanya kazi wataalamu wangu walihitaji vitendea kazi ambavyo nimewawezesha vifaa hivyo zikiwemo Computer 50 katika manispaa zote za Mkoa na kuwataka kutoa vibali ndani ya mwezi Mmoja tangu kupokea maombi kutoka kwa Mwananchi,"amesema.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search