'Wazazi fateni masharti ya kisukari'..soma habari kamili na Matukio360...#share

Na Abraham Ntambara

WAZAZI wenye watoto walio na maradhi ya kisukari wameshauriwa kuhakikisha wanawahudumia kwa kuzingatia ushauri wa madaktari hususani katika vyakula ili maisha yao yawe salama.
Msimamizi wa Mradi wa Huduma za  Kisukari kwa Watoto nchini Herieh Mganga akizungumza na waandishi wa habari.

Ushauli huo umetolewa leo jijini Dar es Salaam na Msimamizi wa Mradi wa Huduma za  Kisukari kwa Watoto nchini Herieh Mganga wakati wa zoezi la kupima wanafunzi wa shule ya sekondari ya wasichana Kisutu ili kubani kama wanaviashiria vya ugonjwa wa kisukari.

Zoezi hilo amablo limeratibiwa na Chama cha Wagonjwa wa Kisukari nchini kwa Kushirikiana na Chama cha Magonjwa yasiyo ya kuambukiza, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto na Tamisemi lengo ni kufikia watoto wa kike katika maeneo mbali mbali nchini na kuwajengea ufahamu juu ya uwepo wa uwepo wa watoto wenye ugonjwa wa kisukari.

Amesema watu wengi wamekuwa wakifariki kwa ugonjwa huo kutokana na kukosa elimu ya jinsi ya kukabiliana nao.
“kwa hiyo hapa tupo tunapima urefu, uzito na mapigo ya moyo, tunapima haya ili kujua kama kunaviashiria vya ugonjwa wa kisukari na magonjwa yasiyo ya kuambukiza,” amesema.

Aidha ameeleza kuwa  tatizo hilo ni kubwa na kubainisha kuwa hadi sasa wamekwishaandikisha vijana Zaidi ya 2488 wenye ugonjwa huo katika kilniki 34 ambazo wanazsimamia.
Mmoja wa vijana wanachama wa Chama cha Vijana wenye kisukari nchini (TBYA) Anita Bulindi akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Anita Bulindi ambaye ni mmoja wa vijana ambao ni wanachama wa Chma cha Vijana wenye Kisukari nchini (TBYA) amewataka wazazi kuamini kuwa hata watoto wanaweza kupata maradhi hayo na kuwataka wanapokutana na hali hiyo waione kama hali ya kawaida.
Mwalimu Mkuu wa shule ya sekondari ya wasichana Kisutu jijini Dar es Salaam, Sylvia Lymo akizungumza na waandishi wa habari.

Kwa upende wake Mwalimu Mkuu wa Shule ya Kisutu Sylvia Lyimo amesema zoezi la kupima afya za wanafunzi ni zuri na ameshauri waende kufanya huduma hiyo na katika shule nyingine.







About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search