Naibu Waziri atembelea TAWA... soma habari kamili na Matukio360... #share



Dkt. Felician Kilahama (Mwenyekiti wa Bodi TAFORI) Naibu Waziri Maliasili na Utalii Japhet Ngailonga Hasunge mbele ya watumishi wa TAWA na TAFORI

Mhe. Japhet Ngailonga Hasunge (Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii) wa kwanza kutoka kushoto waliyoka akiwa kwenye picha ya pamoja na Dkt. Stephene Kabwe (Mkuu wa Mkoa wa Morogoro) wa pili kutoka kushoto waliyoka. Waliyosimama wa kwanza kushoto ni Bw.David Kanyatta, wa pilikutoka kushoto ni Dkt.James Wakibara (Kaimu Mkurugenzi Mkuu-TAWA), wa tatu ni Bw. Chuwa (Afisa Maliasili Mkoa wa Morogoror); wanne ni Bw. Edgar Masunga (Kaimu Mtendaji Mkuu –TTSA), na wa mwisho ni Bw. Kaisi Mwaikambo (Kaimu Mkkurugenzi Mkuu-TAFORI)

Mhe. Naibu Waziri kabla ya kuongea na watumishi wa TAWA alifika ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro kwa ajili ya kujitambulisha kwake na kupokea taarifa fupi kutoka kwa Dkt.Stephene Kebwe( Mkuu wa Mkoa wa Morogoro). Kikao hicho kilihudhuriwa pia na Dkt.James Wakibara (Kaimu Mkurugenzi Mkuu-TAWA), Edgar Masunga (Kaimu Mtendaji Mkuu –TTSA), Kaisi Mwaikambo (Kaimu Mkurugenzi Mkuu-TAFORI) na Bw.David Kanyatta (Kaimu Mkurugezi Huduma za Raslimari wanyamapori –TAWA). Mkuu wa Mkoa  alimueleza Naibu Waziri  kwamba Mkoa wa Morogoro umebalikiwa kuwa na Hifadhi nyingi za Wanyamapori ikiwemo Pori la akiba kuliko yote barani Afrika, Pori la Selous.
Mkuu wa Mkoa alisema, hifadhi hizo zina changamoto nyingi sana hasa suala la kuingiza ng’ombe ndani ya Mapori hayo. Aidha Uongozi wa Mkoa unajitahidi kufanya operesheni za kuondoa mifugo kwa kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama pamoja na Hifadhi za Taifa (TANAPA), Wakala wa Huduma za misitu(TFS), na Mamlaka ya Usimamizi wanyamapori Tanzania (TAWA). Mfano amezungumzia  operesheni ya hivi karibuni iliyofanyika katika  Hifadhi za Jumuhiya ya jamii za Wanyamapori (WMA) kwa kuondoa mifugo, na kuchoma nyumba za makazi zaidi ya 1,069 zimevunjwa.Akizungumzia Bonde la Mto Kilombero, amesema vilevile amefanya operesheni ya kuondoa mifugo katika Bonde la Kilombero .
Mhe. Japhet Ngailonga Hasunge (Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii)

Dkt.Stephene Kabwe (Kulia) akimueleza jambo Naibu Waziri mbele ya watumishi wa TAWA na Mkuu wa Mkoa ofisini kwake Morogoro.

Dkt.KJames Wakibara(wa nne kushoto), Bw.Edgar Masunga (wa tatu kutoka kushoto), Bw.Kaisi Mwaikambo (wa pili kushoto) na Bw. David Kanyatta (wa Kwanzaa kushoto)
Naibu waziri asifu juhudi zinazofanywa na Mkoa wa Morogoro katika kukabiliana na changamoto mbalimbali za uhifadhi. Pia alimshukuru Mhe. Rais kwa kumteua kushika nafasio hiyo. Alimueleza Mkuu wa Mkoa kuwa Wizara ya Malaisili na Utalii ina majukumu ya kutangaza utalii wa ndani na nje ya nchi, kuhakikisha raslimari za wanyamapori zinalindwa,na amesemaWizara inajikita kujitangaza zaidi utalii wa kusini mwa Tanzania.
Naibu waziri baada ya kusalimiana na Mkuu wa Mkoa alitembelea ofisi za TAWA Makao Makuu na kusaini kitabu cha wageni na baadaye kuongea na watumishi. Kabla ya kuanza hotuba yake alikaribishwa na Dkt. James Wakibara (Kaimu mkurugenzi Mkuu-TAWA) kwa kumueleze mambo machache kuhusu TAWA.
Naibu Waziri akisalimiana na Bw. Chuwa (Afisa Malaisili wa Mkoa wa Morogoro) mbele ya Ofisi za Makao Makuu ya TAWA na pembeni  Mkurugenzi Mkuu-TAWA akishuhudia

Naibu anaweka sahihi kitabu cha wageni ofisi ya TAWA

phor

Naibu Waziri akiwa na Mkurugenzi wa TAWA ofisini kwake
Dkt Wakibara alisema’ Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) ni mamlaka iliyoanzishwa kwa Amri ya Serikali na kutangazwa kwenye gazeti la Serikali Na.135 la tarehe 9 Mei, 2014. Uanzishwaji wa Mamlaka hii ni utekelezaji wa kifungu cha 8 cha Sheria ya kuhifadhi Wanyamapori Na. 5 ya mwaka 2009’.

 Dkt.James Wakibara (Mkurugenzi Mkuu-TAWA) akifikiria jambo kwa makini
Dkt Wakibara alitaja malengo makuu ya TAWA:-
        i.            Kuboresha usimamizi wa raslimari za wanyamaspori nje ya hifadhi za Taifa na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro
      ii.            Kuimarisha usimamizi wa wanyamapori
    iii.            Kuboresha ubora na ufanisi wa utendaji kazi
Dkt wakibara alimueleza Naibu waziri kwa kutaja maeneo yanayosimamiwa na TAWA kuwa ni:-
·        Mapori ya Aiba 28 (114,782 km2)
·        Mapori tengefu 42 (56,765 km2)
·        Maeneo ya Ardhioevu (3) (48,634 km2)
Dkt Wakibara kuhusu masuala ya utalii alimueleza Naibu Waziri kuwa TAWA inasimamiwa vitalu vya uwindaji157, ingawa vinachangamoto, vitalu 61 viko wazi; 24 havikupata wawekezaji;47 vilirejeshwa; 54 vimetangazwa upya mwezi Septemba,2017.
Kuhusu suala la ujangili, Dkt.Wakibara  alimueleza Naibu Waziri kuwa juhudi mbalimbali zimekuwa zikifanyika kukabiliana na ujangili na kutoa takwimu ambazo TAWA imefanya tangu kuanzishwa kama ifuatavyo:-
a.     Siku doria 58,580 (66%) zimefanyika
b.     Siraha 112 zilikamatwa zikiwepo SMg 2, Rifle 9 Shotgun 22, Bastola 2, Gobore 87, fataki 54, Risasi 985
c.      Watuhumiwa 889 walikamatwa, kesi 415 zimefunguliwa
d.     Wanyama waharibifu siku doria 4,820 ongezeko la 53.4%, matukio 160.
Akizungumzia mifugo,alimueleza kuwa jumla 14,059 ilikamatwa
·        Ng’ombe 13,865; mbuzi94; punda33; kondo67
·        Mifugo 2,121 iliuzwa kwa amri ya mahakama
·        Mifugo 11,938inaendelewa kushikiliwa
·        Mapori sugu ya mifugo;Maswa,BBK,Moyowosi/Kigosi, Rungwa/Kizigo/Muhesi,Uwanda, Selous,Ikorongo/Grumeti, Swagaswaga, Mkungunero na Kilombero  GCA.
Kuhusu utengenezaji mipaka wa mipaka, jumla ya vigingi 799 viliwekwa katika maeneo mbalimbali.  Katika Mapori ya Akiba 20. (hadi sasa 40%)
Baada ya Hotuba ya Dkt. James Wakibara, alimueleza Naibu Waziri mbali na changamoto mbalimbali za uhifadhi, TAWA imefanikiwa kuongeza mapato yake kutoka Bill 36 hadi 38 kwa mwaka.
 Naibu Waziri akizungumza na watumishi, alisistiza mambo yafuatayo katika hotuba yake:-
                                                                                                        i.  

Aliwashukuru uongozi mzima wa TAWA kwa kazi nzuri za kupambana na ujangili na kulinda raslimari za wanyamapori


ii. Aliwaomba TAWA waongeze mapato kwa kutumia mfumo wa kielekroniki


iii. Aliwapongeza TAWA kwa kujadili na kuandaa Mpango mkakati wa TAWA (Strategic Plan) ambayo iko kwenye hatua za mwisho kumalizika


iv. Amewaomba TAWA kuongeza juhudi za kuanda Sheria ya TAWA ipatikane haraka iwezekanavyo


v. Matarajio ya Serikali ya awamu ya tano ni kuchapa kazi na kwa uadilifu na kuepukana navitendo vya rushwa.


vi. Amewaomba watumishi kuwa wabunifu


vii. Amewaomba watumishi kudhibiti mifugo yote inayoingia Mapori ya Akiba na maeneo mengine ya uhifadhi kwa kufuata sheria. Mifugo yote iondolewe ndani ya hifadhi.


viii. Amesisitiza kuwa Wizara inaweka msisitizo wa jeshi husu kwenye Taasis zake zote


ix. Utoaji wa Elimu kwa wananchi, shuleni,vyuo ni kitu muhimu, waelimishwe kwa njia za mikutano,redio,Tv, vpeperushi na Maonesho ya sinema


x. Aidha ,amesisitiza TAWA waongeze kasi ya kujitangaza hasa masuala ya Utalii


xi. Kufahamishana habari mbalimbali za utendaji (Sharing Information) ni kitu nyeti
Naibu waziri akikaribishwa na Dkt.Felician Kirahama(M/Kiti wa Bodi ya TAFORI) alipowasili kuongea na watumishi wa TAWA.
Baadhi ya watumishi wa TAWA wakimsiliza Naibu Waziri (Hayupo kwenye picha hii)
Watumishi wa TAWA wakimsikiliza
 Bw.Mabula Misungwi (Kaimu Mkurugenzi Huduma za ulinzi wanyamapori-TAWA).
Bw.Nkuwi Richard (Kaimu Mkurugenzi Huduma za Utalii na Biashara-TAWA)
Bw.David Kanyatta (Kaimu Mkurugenzi huduma za raslimari wanyanyamapori-TAWA) wa kushoto.
Bw.Willian Kitebi (Kaimu Mkurugenzi Huduma za TAWA)
 Imeandaliwa na,
Twaha Twaibu
AFISA HABARI NA MAHUSIANO-TAWA

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search