Meneja Peacock mbaroni kwa ushoga..Soma habari kamili na Matukio360...#share

Na Abraham Ntambara

JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linamshikilia Meneja Mkuu wa Hoteli ya  Peacoak kwa kosa la kuhifadhi watu 12 wanaodaiwa kuhamasisha mapenzi ya jinsia moja (Ushoga).


Mkuu wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam ACP Lazaro Mambosasa akizungumza na waandisi wa habari.

Watu hao ni raia wa Afrika Kusini wawili, Uganda mmoja na  Tanzania tisa.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaan  Kamanda wa Kanda hiyo, ACP Lazaro Mambosasa amesema sheria za nchi zinakataza vitendo vya ushoga  na ni kinyume cha utamaduni.

“Kitendo cha kuhamasisha kuingiliana kinyume na maumbile ni kosa la kisheria, vitendo hivyo vya ushoga haviruhusiwi nchini,” amesema ACP Mambosasa.

Amesema mwananchi yeyote Dar es Salaam atakaye hifadhi watu wa jinsi hiyo atakamatwa na kuchukuliwa hatua za kisheria.

Wakati huo huo Jeshi hilo limefanikiwa kukamata Silaha aina ya SMG, Bastola moja aina ya CZ Magazine mbili, risasi 17, Mabomu aina ya Graned  saba, pikipiki moja aina Ferkon na kuuwa majambazi watano wasiotambulika majina.


Katika hatua nyingine, Kamanda Mambosasa ameeleza kupatikana kwa magari ya wizi, vitu mbalimbali vikiwemo laptop 3, simu 100 na kukamatwa kwa watuhumiwa tisa wa wizi huo.

ACP Lazaro Mambosasa akionyesha waandishi wa habari Mabomu aina ya Graned waliyokamata.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search