Waziri Kairuki: Watumishi hewa walininyima usingizi..Soma habari kamili na Matukio360..#share


Na Abraham Ntambara

WAZIRI wa Madini Angella Kairuki amesema suala la uhakiki wa watumishi hewa lilimnyima usingizi katika kipindi alichokuwa Waziri wa Ofisi ya Rais- Utumishi na Utawala Bora.

Waziri wa Madini Angella Kairuki akimkabidhi Kitendea kazi Waziri  Ofisi ya Rais- Utumishi na Utawala Bora, George Mkuchika  jijini Dar es Salaam.

Kairuki amesema hayo leo jijini Dar es Salaam wakati akimkabidhi ofisi Waziri Mpya wa Ofisi ya Rais –Utumishi na Utawala Bora George Mkuchika, amebainisha kuwa ni kutokana na baadha ya Maafisa Utumishi kutokuwa waaminifu kwa kutoa taarifa zisizo sahihi za watumishi.

“Changamoto kubwa niliyokabiliana nayo ni suala la uhakiki wa watumishi, suala kubwa ni baadhi ya Maafisa Utumishi hawakuwa waaminifu katika kutoa taarifa sahihi,” amesema Waziri Kairuki.

Aidha amesema kuwa kwa kipindi chote cha miezi 23 alichokuwa waziri wa Utumishi alikuwa akitengeneza mazingira mazuru kwa kurekebisha na kurejesha nidhamu ya watumishi wa umma katika kutumikia wananchi.

Katika zoezi la uhakiki wa watumishi hewa lililofanywa nchini, zaidi ya watumishi  10295 walibainika kutokuwa na sifa za kuwa watumisshi wa umma.

Kwa upande wake Waziri Mkuchika amesema katika kipindi chake cha kuiongoza wizara hiyo hatavumilia watumishi wazembe watakaoshindwa kukaa mahali pao pakazi muda wa masaa ya kazi ili kuwatumikia wananchi kwa kisingizio cha kwenda mjini kunywa chai.

 “Nitahakikisha watumishi wanawatumikia wananchi kwa nidhamu na mambo ya kizebe sitayakubali, nataka watumishi walipwe mishahara kamili kwa kazi kamili,” amesema Mkuchika.

Amebainisha kuwa watumishi wamekuwa wakilipwa mishahara kamili kwa kazi nusu kwani wamekuwa hawakai ofisini huku akiwataka kutumia kantini zao kwa masuala ya chakula au kutafuta utaratibu mwengine lakini siyo nje ya ofisi.

Katika mwaka wa fedha wa mwaka huu, amesema katika kuboresha maslahi ya watumishi, zaidi ya watumishi 20,0000 watapandishwa madaraja na vyeo.

Aidha amesisitiza kuwa ili kupiga vita suala la rusha wizara yake itahakikisha inatoa elimu ya rushwa kawa wananchi kwani wamekuwa wakitoa rushwa kwa kutokuwa na elimu ya kutosha juu ya masuala hayo.

Waziri wa Madidi Angella Kairuki na  Waziri wa Ofisi ya Rais- Utumishi na Utawala Bora George Mkuchika Wakizungumza na waandishi wa habari wakati wa makabidhiano ya ofisi leo jijini Dar es Salaam.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search