Waziri Mwijage mgeni rasmi tamasha la maonesho ya magari..Soma habari kamili na Matukio360..#share

Na Salha Mohamed

WAZIRI wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika tamasha la maonesho ya magari litakalofanyika Oktoba 27 hadi 29, 2017 jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Vision Investiment, Ally Nchahaga (katikati) akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maonesho ya 10 ya tamasha la magari litakalozinduliwa na Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage Oktoba 27,The Green jijini Dar es Salaam.

Maonesho hayo ya siku tatu yameandaliwa na Kampuni ya New Vision yatafanyika katika viwanja vya The Green, lengo likiwa kuonesha bidhaa za vyombo vya moto na huduma kwenye vyombo vya moto,kupata elimu na kuridhishwa navyo.

Akizungumza na waandishi wa Habari leo jijini Dar es Salaam, Mratibu wa Maonesho hayo, Ally Nchahaga amesema maonesho hayo yatafungwa Oktoba 29 na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Ally Hapi.

"Tuko hili linahusisha moja ya maonesho muhimu sana na enye mvuto katika ulimwengu wa vyombo vya moto,matoleo mapya ya pikipiki na burudani kwa ajili ya familia,"amesema.

Amesema watu wengi wanashindwa utunzaji sahihi wa magari kutokana na kukosa elimu kwan magari ya sasa mengi hutuma teknolojia na si kama ya zamani.

Nchahaga amesema tamasha hilo ni muhmu katka vyombo vya moto kwa kuonesha magari ya abiria, biashara, pikipiki, bodi za magari, sehemu za magari, mashine, huduma shirikishi na zana zinazohusika na magari.

Amesema katika maonesho hayo kutakuwa na burudani ambapo wapenzi wa magari wataonesha ujuzi wa kucheza na vyombo vya moto ambayo itawaburudisha watoto na kuwaelimisha usalama barabarani.

Kwa upande wake mdhamini wa Tamasha hilo ambaye pia ni Meneja Mauzo wa  Kampuni ya Bima ya Britam, Oscar Ruhasha amesema watatoa elimu ya bima kwa vyombo vya moto kwani watu wengi hawana elimu hiyo.



Ofisa Masoko wa Kampuni ya kuuza magari ya Hyundai, Anthony Nyeupe amesema kupitia tamasha hilo wananchi watapata fursa ya kubadilishana mawazo na kuonesha bidhaa zao mpya.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search