Kesi ya uchochezi ya Lema kusikilizwa kwa siku 3 mfululizo..Soma habari kamili na Matukio360..#share
KESI ya Uchochezi inayomkabili Mbunge wa Arusha Mjini kwa
tiketi ya Chama cha Demkrasia na Mendeleo (Chadema) Godbless Lema inatarajiwa
kusikilizwa mfululizo kwa siku tatu katika Mahakama ya Wilaya ya Arusha.
Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema
Hayo yemebainishwa leo na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama
hiyo, Devota Msoffe, amesema kutokana na kesi hiyo kuwa nje ya wakati, itasikilizwa kuanzia Novemba 27 hadi 29, 2017 ambapo upande wa Jamhuri ndiyo utakaoanza
kuleta mashahidi wao.
“Tutasikiliza kesi hii siku tatu mfululizo kwani iko nje ya
wakati na natoa agizo kwa mashahidi wa Jamhuri kuitwa ambapo tunatarajia
kufunga ushahidi wao Novemba 29,” alisema Hakimu huyo.
Hatua hiyo inakuja baada ya jana upande wa Jamhuri kumsomea
maelezo ya awali mshtakiwa huyo ambaye pia anakabiliwa na kesi nyingine ya
uchochezi katika Mahakama ya Wilaya ya Arumeru.
Wakili wa Serikali, Agness Hyera, akimsomea Lema maelezo ya
awali katika kesi hiyo namba 440 ya mwaka 2016, alidai kuwa mshtakiwa huyo
anakabiliwa na shtaka moja la uchochezi ambapo anadaiwa kutenda kosa hilo
Oktoba 22, mwaka jana katika eneo la Kambi ya Fisi, Kata ya Ngarenaro akiwa
anahutubia mkutano wa hadhara.
Miongoni mwa maneno ya uchochezi anayodaiwa kuyatoa Lema ni pamoja na: “Rais Magufuli akiendelea na tabia ya kudhalilisha demokrasia na uongozi wa upinzani iko siku Taifa litaingia kwenye umwagaji wa damu,…. “Rais yeyote ambaye haheshimu mipaka ya sheria, mipaka ya Katiba, rais huyo ataliingiza Taifa katika majanga na umwagaji damu,watu watajaa vifua, wakiamua kulipuka polisi hawa wala jeshi halitaweza kudhibiti uhalifu utakaojitokeza.”
Baada ya kumsomea mashtaka hayo, Wakili Hyera aliiomba mahakama kupanga tarehe ya kuanza kusikiliza na kuwa hawakuwa tayari kuweka hadharani majina ya mashahidi wao wala vielelezo ambapo alisema wanatarajia kuwa na mashahidi wasiozidi 10.
Miongoni mwa maneno ya uchochezi anayodaiwa kuyatoa Lema ni pamoja na: “Rais Magufuli akiendelea na tabia ya kudhalilisha demokrasia na uongozi wa upinzani iko siku Taifa litaingia kwenye umwagaji wa damu,…. “Rais yeyote ambaye haheshimu mipaka ya sheria, mipaka ya Katiba, rais huyo ataliingiza Taifa katika majanga na umwagaji damu,watu watajaa vifua, wakiamua kulipuka polisi hawa wala jeshi halitaweza kudhibiti uhalifu utakaojitokeza.”
Baada ya kumsomea mashtaka hayo, Wakili Hyera aliiomba mahakama kupanga tarehe ya kuanza kusikiliza na kuwa hawakuwa tayari kuweka hadharani majina ya mashahidi wao wala vielelezo ambapo alisema wanatarajia kuwa na mashahidi wasiozidi 10.
No comments:
Post a Comment