Zitto; Serikali 'inapika' Takwimu pato la taifa(GDP)...soma habari kamili na Matukio360...#share
Na
Saha Mohamed
KAMATI Kuu ya Chama cha ACT Wazalendo,
imesema takwimu za ukuaji wa pato la taifa(GDP)zimepikwa na si sahihi kama ambavyo taasisi za serikali
zikidai.
Hayo
yamebainishwa leo jijini Dar es Salaam na kiongozi wa Chama hicho, Zitto Kabwe
wakati akiwasilisha ushahidi kuhusu kusinyaa kwa uchumi wa nchi.
Amesema Mkaguzi wa Hesabu za Serikali(CAG),
anapaswa kufanya ukaguzi wa mapato ya serikali kwa Julai na Agosti mwaka huu na kuiweka wazi kwa umma.
Amesema mbali na CAG kufanya ukaguzi pia
Mamlaka ya Mapato (TRA) ieleze mapato yake kwa kila idara pamoja na kuonesha
marejesho na madeni yatakayokusanywa kama mapato.
Zitto ambaye pia ni mbunge wa jimbo la Kigoma
mjini amesema Jumuia za Afrika Mashariki, Benki ya Maendeleo ya Afrika na Benki
ya Dunia kufanya uchunguzi maalumu wa takwimu za uchumi nchini.
“Hatua kali zichukuliwe dhidi ya serikali ya
awamu ya tano ikigundulika kuwa takwimu juu ya ukuaji wa pato la taifa
zimepikwa,”amesema zitto.
Ameongeza kuwa Serikali inapaswa kubadilisha
sera zake za matumizi kwa kuhakikisha miradi mikubwa inayotekelezwa nchini
inaingiza fedha nchini na si kupeleka fedha nje ya nchi kama ambavyo imenunua
ndege 6 kwa fedha taslimu.
Amesema kwa kufanya hivyo kunaonesha madhara
kwenye uchumi kwasababu badala ya kuongeza mzunguko wa fedha kwenye uchumi
unafanya uchumi kusinyaa.
Amesema Pato la taifa ndiyo kipimo cha afya
au uhai wa uchumi wa taifa kwani ukuaji
au uporomokaji wake hutumika kupima shughuli za kiuchumi za taifa husika.
Ameongeza kuwa tafiti zinaonesha ili
kuondokana na umasikini wa nchi, uchumi unatakiwa ukue kwa kiwango cha tarakimu
mbili kwa miaka mitano mfululizo kiwango hicho hakijawahi kufika.
Amesema wastani wa ukuaji umekuwa kwa asilimia 7 huku katika mzunguko
wa fedha kwa miaka mitano iliyopita umekuwa kati ya asilimia 0.5 na 1.5.
Zitto amesema kiwango hicho hakitofautiani na
kiwango ambacho Benki Kuu ya Ulaya(ECB)imeweka kama mzunguko wa ujazo wa fedha
kwa nchi zote za Umoja wa Ulaya(EU).
Amefafanua kuwa takwimu za mwaka 2014 hadi
2016 za ukuaji wa GDP robo ya pili Aprili hadi Juni ya kila mwaka zimekuwa
zikishabihiana.
“Hali hiyo imekuwa tofauti mno kwa robo ya
pili ya mwaka 2017, utofauti ambao mdiyo msingi ulioibua shaka na kusababisha utafiti
huu,”amesema.
Amesema robo ya pili ya mwaka 2017 Benki ya
Kuu(BOT) imetoa takwimu za ukuaji wa GDP kwa robo inayoishia Juni 2017 kukua
kwa kasi ya asilimia 5.7 na mfumuko wa bei asilimia 6 ambapo kasi hiyo
unatofautiana na mlinganisho wa kanuni za kiuchumi.
“Mtakubaliana name kuwa takwimu za pato la taifa kwa robo inayoishia Juni
2017 si takwimu sahihi, hazikubaliani na nadharia ya uchumi na zimetofautiana
sana na miaka minne ya nyuma,”amesema.
Zitto ameongeza “Takwimu hizi zimepikwa ili
kuonesha picha kua hali ya uchumi ni nzuri ilhali uhalisia ni kwamba kasi ya
ukuaji wa uchumi imeporomoka mno,”amesema.
Amesema kwa miezi kadhaa wamekuwa wakipiga
kelele kuwa kitendo cha serikali kuminya sekta ya fedha na hasa kwa sekta
binafsi.
Ameongeza kuwa takwimu za makusanyo ya kodi
za serikali kutoka TRA, zinaacha mashaka makubwa kwa kila mtaalamu wa uchumi na
kuamini kuwa ni za kutengezezwa.
“Julai, serikali ilikusanya sh bilioni 390
kutoka kodi za forodha, lakini Julai serikali haikuwa na takwimu za biashara ya
kimataifa kwa sababu mfumo wa forodha ya pamoja katika EAC.
“Je serikali imewezaje kupata takwimu za kodi
bila takwimu za biashara?kodi inatoka kwenye bidhaa zilizoingizwa nchini hivyo
ili kupata kodi lazima kupata bidhaa kwanza,ni dhahiri serikali inaficha
takwimu hizi makusudi ili kuzuia kuonesha kuwa mapato yameshuka,”amesema.
No comments:
Post a Comment