BAKWATA:Sensa si mfarakano...soma habari kamilli na Matukio360..#share

Salha Mohamed
UMOJA wa Vijana wa Baraza Kuu la Waislamu Taifa (Bakwata), limewatoa hofu waislamu wanaodhani mchakato wa sensa kwa waislamu ni chanzo cha mfarakano wa taifa.


Katibu Umoja wa Vijana wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata), Sheikh Othman Zuberi akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati akitoa tamko la kumpongeza na kumuunga mkono utendaji kazi wa Mufti Mkuu wa Tanzania, Sheikh Abubakar Zuberi jijini Dar es Salaam.

Hayo yamesemwa jijini Dar es Salaam na Katibu wa Umoja huo, Sheikh Othman Zuberi wakati wa kutoa tamko la pongezi na kuunga mkono utendaji kazi wa Mufti Mkuu wa Tanzania, Abubakar Zuberi katika kipindi cha miaka miwili.

Amesema sensa kwa maendeleo ya waislamu inafaa jambo linaloonesha umakini wa kuwatumikia waislamu na kutoa huduma kwa usahihi kwa watu anaowatumikia.

"Hivi karibuni Mufti aliwaagiza makatibu wa Baraza kujiandaa na sensa ya waislamu, msikiti na madrasa kote nchini, "amesema.

Amewatoa hofu vijana  nchini wanaoona mchakato huo unaweza kuwa chanzo cha mfarakano wa taifa kiimani.

" Hasha wa kala haiwezi kuwa hivyo kwani tunavyomfahamu Mufti ni mwenye kuongoza na qur-an na hadithi za mtume vyanzo ambavyo vimejaa mahimizo ya mshikamano,"amesema.

Ameongeza kuwa kufanya sensa kwa waislamu ni ibada huku akisisitiza haiwezi kuwa chanzo cha mfarakano baina yao na kwamba inaleta maendeleo kwa waislamu.

Amesema katika kipindi cha miaka miwili, Mufti amefanikiwa kupata wahisani wa kujenga ofisi za kisasa za Bakwata na kuonesha ushirikiano baina ya waislamu na waislamu waislamu pamoja na waislamu na wasiokuwa waislamu.

"Tulizoea kuona mafarakano na kashfa za wazi baina ya makundi lakini sasa yamepungua kwa kiasi kikubwa au hayapo kabisa, "amesema.


Ameziomba taasisi za dini nchini kumuunga mkono Mufti katika mema anayoyafanya kwa maslahi ya waislamu na taifa kwa ujumla.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search