Waziri Mkuu: Katiba mpya bado, amzungumzia Tundu Lissu...soma habari kamili na Matukio360..#share
Na mwandishi wetu
SERIKALI imesema kwa sasa
mchakato wa kuendelea na upatikanaji wa katiba mpya si kipaumbele chake kwa kuwa unahitaji fedha nyingi.
Msimamo huo umetolewa leo
Bungeni Dodoma na waziri mkuu, Kassim Majaliwa katika kipindi cha maswali na
majibu ya ana kwa ana na waziri huyo.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, akijibu majibu Bungeni Dodoma
Akijibu swali la Mbunge wa
Temeke, Abdallah Mtolea kuhusu Katiba mpya, waziri mkuu amesema kwa sasa kipaumbele
cha serikali ni kuboresha huduma za
jamii .
‘Tatizo ni kuwa mchakato wa
upatikanaji wa katiba mpya unahitaji fedha nyingi na kwa sasa kipaumbele cha serikali ni kuboresha
huduma za jamii, hivyo haiwezi kuratibu suala hilo,’ amesema
Amesema suala hilo pia
linashindikana kutokana na bajeti ya
mwaka 2017/18 haikuelekeza wala kutoa kipaumbele kwenye mchakato wa upatikanaji wa katiba
mpya.
Kuhusu upelelezi wa tukio la
upigwaji risasi mbunge Tundu Lissu amesema suala hilo bado linaendelea
kuchunguzwa na vyombo vya usalama vya ndani na kwamba serikali kwa sasa haiwezi
kuruhusu vyombo vingine vya nje kuchunguza suala hilo.
Alikuwa akijibu swali la
mbunge wa Hai(Chadema) Freeman Mbowe ambaye pia ni mwenyekiti taifa wa chama
hicho, aliyetaka serikali kuruhusu vyombo huru kutoka nje ya Tanzania
kuchunguza tukio hilo.
Waziri Mkuu amesema kwa sasa
hawezi kutoa uamuzi wowote hadi hapo
vyombo vya usalama vitakapomaliza uchunguzu na kutoa mapendekezo yao.
Kuhusu zao la mbaazi, waziri
mkuu amesema serikali inaendelea na jitihada za kutafuta masoko na kwamba
ilikuwa ikitegemea nchi ya India pekee kununua zao hilo.
‘Lakini kwa mwaka huu India
imezalisha ziada ya asilimia 30 ya mbaazi hivyo imezuia kununua mbaazi kutoka
nje. Lakini pamoja na changamoto hiyo serikali inaendelea kutafuta soko mahala
pengine,’amesema
Binafsi, ninahoji majibu ya Waziri Mkuu. Hii hoja ya gharama kuhusiana na katiba mpya nina mashaka nayo. Ingekuwa serikali ina uchungu na hela za walipa kodi, mbona haisemi ni gharama kuwadhibiti wapinzani wanapotaka kutumia haki zao kwa mujibu wa katiba na sheria? Mpinzani akiikosoa serikali, hata kama yuko mbali kiasi gani, anatafutwa na magari ya polisi wenye silaha na kubebwa hadi kituoni. Wapinzani wakikusanyika kwa mujibu wa katiba na sheria ya vyama, mabomu ya kuwatawanya yako tele, hata kwenye miji midogo. Magari ya maji ya washawasha ya kuwatawanya yako tele. Mafuta ya haya magari, spea za haya magazi, posho za madereva na polisi, nazo si gharama? Hao watu wanaoitwa wachochezi wanafunguliwa kesi kila kukicha, kesi ambazo wanashinda, kwa sababu hazina vichwa wala miguu. Lakini hela za walipa kodi zinafujwa katika kesi hizo. Ufujaji huu wa hela unaofanywa na serikali unanifanya niwe na mashaka na hoja ya waziri mkuu kuhusu gharama ya kuendelea na mchakato wa katiba mpya.
ReplyDeleteKuhusu suala la uchunguzi wa tukio la kushambuliwa kwa Tundu Lissu, nimesikia kuwa familia ya Tungu Lissu, pamoja na kuwa wanataka wachunguzi wa ndani wafanye hiyo kazi, wanataka wachunguzi wa nje washirikishwe. Serikali itumie busara kwenye suala hili. Ili kuondoa mashaka na tuhuma dhidi yake, ni busara kujumlisha wachunguzi wa nje. Itaondoa wingu lot. Ila kama serikali haijali minong'ono na hisia dhidi yake, basi iendelee hivyo inavyotaka.