Bwakata yaendelea kusaka mali za waislam kimya kimya...soma habari kamili na Matukio360..#share

 Na Salha Mohamed
 SHEIKH Mkuu wa Tanzania, Abubakar Zuberi anaendelea kufuatilia mali za waislamu kimya kimya ili aweze kufanikiwa kuzipata.

Katibu Umoja wa Vijana wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata), Sheikh Othman Zuberi akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati akitoa tamko la kumpongeza na kumuunga mkono utendaji kazi wa Mufti Mkuu wa Tanzania, Sheikh Abubakar Zuberi leo jijini Dar es Salaam.

Hayo yameelezwa leo Dar es Salaam  na Katibu wa Umoja wa Vijana Bakwata Taifa, Sheikh Othman Zuberi wakati akizungumza na waandishi wa habari.

Amesema tangu Sheikh Zuberi alipochaguliwa Septemba 10,2015 alianza msako wa mali za waislamu. Amesema waislamu waondoe wasiwasi mali zao kwani muda si mrefu matunda ya mali hizo yataonekana.

"Akiwa na muda mfupi mno tangu alipochaguliwa, Mufti alianza msako wa mali za waislamu jambo ambalo analifuatilia kwa umakini na uangalizi wa hali ya juu, "amesema.

Amesema muda si mrefu waislamu wataanza kuona matunda yake kwani anafuatilia kimya kimya na kwa umakini.


" Utaratibu wa urejeshaji wa mali za Baraza zilizopotea unaendelea kufanyika, baraza limefanya ukaguzi na uboreshaji wa shule, kuanzisha daaru (maarif ya kujifunzia elimu zote za dini,  kusimamia sera ya mahusiano mazuri baina ya waislamu, "amesema.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search