Kigamboni marathon Disemba 2, 2017...Soma habari kamili na Matukio360..#share

KATIKA jitihada za kuijengea Jamii uelewa na hamasa juu ya  umuhimu wa kutunza afya na Kufanya Mazoezi,  Kampuni ya Events World  kwa kushirikiana na wadau mbali mbali imeandaa mbio za ‘Kigamboni Marathon’ zinazotarajia kufanyika Disemba 2, 2017.



Mratibu Mwenza wa Shindano la Kigamboni Marathoni,Dimo Debwe Mitiki akiwaonesha wana Habari Zawadi zitakazogawiwa kwa washindi wa mbio hizo zinazotarajiwa kufanyika Desemba 2 mwaka huu katika fukwe za Kigamboni jijini Dar es Salaaam

Mbio hizo zitaambatana na zoezi la Upimaji wa afya katika kuadhimisha siku ya Ukimwi Duniani ambayo huazimishwa  Desemba 1 ya kila mwaka.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam Mkurugenzi wa  kampuni Events World  Dimo Mitiki, amesema lengokuu  la mbio hizo ni   kutangaza  fursa za  uwekezaji,  vivutio vya kitalii na biashara zilizopo Kigamboni kwa maendeleo ya Taifa letu.

Aidha ameongeza kuwa zinafanyika ili kuunga mkono kampeni ya Makamu  wa  Rais  Samia Suluhu Hassan   katika kuhamasisha Watanzania kufanya mazoezi ili kuimarisha afya.

“Pia kwa siku za hivi karibuni tumeshuhudia viongozi wetu wakihamasisha wafanyabiashara na wadau mbali kuwekeza ndani ya wilaya yetu mpya ya Kigamboni, hivyo ni imani yetu kuwa kufanyika kwa ‘Kigamboni Marathon’ kutawavutia watu mbali mbali kufika Kigamboni na kujionea uzuri pamoja na fursa zilizopo kigamboni,” amesema Mitiki.

Naye Mratibu wa mbio hizo Juma  Mtetwa amesema kuwa Kigamboni imezungukwa na maeneo mazuri ya kimichezo, Utalii na Uwekezaji kuliko sehemu yeyote Jijini Dar es saalam.

Amesema, hiyo ni sababu moja wapo inayowasukuma kuamini kuwa ‘Kigamboni Marathon’ itakuwa ni miongoni mwa mbio bora zaidi nchini itakayoibua wakimbiaji wazuri watakao leta ushindani mkubwa katika mchezo huu wa riadha Duniani kote. 

“Kigamboni Marathon inatarajiwa kufanyika katika viwanja vya mji mwema jirani na ofisi za Halmashauri mpya ya kigamboni Disemba 2, 2017, kutakuwa na mbio za urefu wa kilomita 21(Half Marathon), kilomita 10 na mbio kwaajili ya watoto, wazee na hata wale wasio na mazoezi ya mara kwa mara (Fun Run) pia zawadi mbali mbali kushindaniwa zikiwemo Medali za dhahabu, Silver na gold pia pesa taslimu kwa washindi,” amesema.

Kwa niaba ya Kamati ya maandalizi ya ‘kigamboni Marathon’ amewashukuru wadau wote waliojitokeza kuunga mkono katika Jambo hili lenye tija kwa Maendeleo ya Taifa  wakiwemo viongozi wa ndani na nje ya Kigamboni, wanahabari, taasisi mbali mbali, kampuni na jamii.

Pia alizishukuru kampuni zilizojitokeza kudhamini mbio hizo ikiwemo Property International, Itel Mobile, Coca cola kupitia kinywaji cha Dasani, J.P.M Hospital, Akemi Restaurant, PCMC Hospital na Red Bull na kuomba wadau na makampumi mbali mbali kujitokeza na ku- support mbio hizo.

Amesema ushiriki wa kampuni kubwa kutoka ndani na nje ya Kigamboni unatoa fursa kwa wafanyabiashara waliyopo Kigamboni na amewasihi wanakigamboni kuitumia fursa hiyo kujumuika pamoja na kuonyesha walichonacho lakini pia kufahamiana na kuongeza Marafiki wenye tija.


Aidha amewakaribisha kuwakaribisha wadhamini, washiriki na wadau mbalimbali kuhudhuria katika tukio hilo la kipekee.




About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search