Dk Shika kuunguruma Desemba 9...soma habari kamili na matukio360..#share

Na Hussein Ndubikile

‘BILIONEA’ wa nyumba za mfanyabiashara Said Lugumi, Dk Luis Shika anatarajia kutoa simulizi ya maisha yake katika hafla maalum ya usiku wa 900 itapendeza itakayofanyika Desemba 9, 2017.
Meneja wa Dk Luis Shika, Catherine Kahabi katikati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaa, wa kwanza kulia ni Dk. Shika na kwanza kushoto meneja burudani Rajab Mteta.

Hayo yamesemwa leo jijini Dar es Salaam na Meneja wa dokta huyo, Catherine Kahabi wakati akizungumza na wanahabari kuhusiana na hafla hiyo.

"Dk. Shika ataongea historia yake alipotoka na mpaka alipo pia kutakuwepo burudani kwa wananchi watakaohudhuria," amesema.

Amesema lengo la hafla hiyo ni kumtambulisha Dk. Shika kama miongoni mwa watu walioupata umaarufu kwa muda mfupi, kumpongeza kwa kushinda mnada wa nyumba za tajiri Lugumi na kumuweka rasmi kwenye muonekano wa u bilionea.

Catherine amesema katika tukio hilo mgeni rasmi anatarajia kuwa aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Lawrence Mashi na itahudhuriwa na watu zaidi ya 5,000.

Kwa upande wake, Dk Shika amewaomba wananchi kujitokeza kwa wingi kusikiliza mambo mengi atakayoyaongea kuhusiana na historia yake.

Naye Meneja Burudani wa ukumbi huo, Rajab Mteta amesema hafla hiyo itasindikizwa na bendi mbalimbali ikiwemo Twanga Pepeta, Jahazi Modern Taarab, wasanii wa Bongo Fleva akiwemo Juma Nature pamoja na mchekeshaji maarufu, Mc Pilipili.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search