Habari katika picha: Yaliyojiri leo bungeni mjini Dodoma...na Matukio360..#share


 

Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,  Mhe. Dk. Tulia Ackson akitoa majibu ya miongozo  mbalimbali  ya wabunge  wakati  wa Mkutano wa tisa wa kikao cha sita  cha  Bunge hilo leo Mkoani Dodoma.


Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dk Ndugulile  akijibu maswali mbalimbali ya wabunge  wakati wa Mkutano wa tisa kikao cha sita cha Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Dodoma.


Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dk. Harrison Mwakyembe  akisoma kauli yake kuhusu fursa kwa wasichana kujipima uwezo katika riadha ili waweze kuiwakilisha nchi katika mashindano yajayo ya kimataifa ya Jumuiya ya Madola, Olimpiki, All-African games na mengineyo leo Bungeni mjini Dodoma.


Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa  na Michezo Mhe. Juliana Shonza akiteta jambo na Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhe. Jumaa Aweso wakati wa Mkutano wa tisa kikao cha sita cha Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Dodoma.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama akizungumza jambo na Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe.Dk. Mary Mwanjelwa wakati wa Mkutano wa tisa kikao cha sita cha Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Dodoma.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search