Mkuu wa mkoa apiga marufuku kuzungumzia ukame...Soma habari kamili na Matukio360..#share

WAKAZI wa Mkoa wa Dodoma wamepigwa marufuku kuzuangumzia suala la ukame.


Mkuu wa Mkoa Dodoma Dk. Binilith Mahenge

Pia amewataka watumishi kuwapa elimu wakulima ili walime mazao yanayostahimili ukame.

Marufuku hiyo imetolewa leo na Mkuu wa Mkoa huo Dk. Binilith Mahenge alipokuwa akizungumza na watumishi wa wilaya ya Chemba, amesema mkoa huo unafaa kilimo cha mazao mengi.

“Kutamka ukame ni kisingizio cha uvivu na ni sawa na watu wasiokuwa na maono, mkoa huu unafaa katika kilimo cha mazao mengi ,” amesema Dk. Mahenge.

Aidha amewaagiza wakuu wa wilaya kuhakikisha wanashughulikia matatizo mengine lakini isiwe katika suala la njaa.

Awali Mkuu wa Wilaya ya Chemba, Simon Odunga amesema wilaya yake imeweka mikakati ya kujitosheleza kwa chakula na  kumaliza migogoro ambayo hupunguza muda wa uzalishaji.

Odunga amesema Chemba imejidhatiti kupambana na upungufu wa chakula na wanayo ardhi ya kutosha kwa ajili ya kilimo.

"Hata hivyo tumeainisha mazao yanayotakiwa kulimwa kwa kila kata kutokana na mtawanyiko wa mvua za msimu," amesema Odunga.

Hata hivyo mkuu huyo amesema kuwa tofauti na maeneo mengine, Chemba wameendelea kukaribisha mifugo kwa kuwa ndiyo fursa kwao katika kuchangia maendeleo.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma, Rehema Madenge amesema mambo mengi yatafanikiwa ikiwa watumishi watafuata utaratibu na kutimiza wajibu wao.

Kwa mujibu wa Madenge bila ya kufuata utaratibu mzuri wa kiusimamizi hakuna kinachoweza kubadilika mkoani humo.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search